Imelda Mtema na Musa Mateja
MSIBA! Staa mwenye umri mdogo
anayekimbiza katika filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amepata pigo
baada ya
kufiwa na bibi yake mzaa mama, Leonadina Mboneko, aliyefariki
dunia juzi asubuhi katika Hospitali ya Masana, iliyopo Mbezi jijini Dar
es Salaam.
Akizungumza na Amani
mama mzazi wa Lulu, Lucresia Karugila alisema mama yake alikuwa
akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu jambo lililomlazimu
kumtoa nyumbani kwake Bukoba na kumleta jijini kwa ajili ya kupata
matibabu.
“Nimehangaika naye kwa muda mrefu ili
kurejesha afya yake, lakini hali ilikuwa ngumu hadi juzi Mwenyezi Mungu
alipomchukua. Tumepata pigo kubwa sana hasa mwanangu Lulu kwa sababu
alikuwa ndiye kipenzi chake,” alisema mama huyo.
Muigizaji huyo aliyecheza Filamu ya
Foolish Age hakuweza kupatikana kuzungumzia msiba wa kipenzi chake huyo,
lakini nyumbani kwa mama yake, mipango ya kusafirisha mwili huo kwenda
Bukoba, Kagera kwa ajili ya mazishi ilikuwa ikifanyika.
Chanzo: GPL


Post a Comment