MUIMBAJI
maarufu hapa nchini wa nyimbo za Injili, Rose Muhando anatafutwa na
waandaaji wa tamasha la Injili wilayani Simanjiro mkoani Manyara kwa
madai ya kutoonekana kutumbuiza kama jinsi walivyokubaliana.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana, Zephania Simoni ambaye ni Mjumbe wa Kamati
ya Uratibu alisema wameingia hasara ya Sh milioni 4.3 kutokana na
tamasha hilo kuvurugika baada ya kutapeliwa na Muhando.
Alifafanua
kuwa tayari walikuwa wameishamkabidhi kiasi cha Sh 1,700,000 muimbaji
huyo na ameshindwa kufika na hivyo kuonesha wazi kuwa amewatapeli
Post a Comment