
Tunaomba kuueleza umma wa Watanzania kuwa Mheshimiwa Makamu wa Rais
hajapanga tukio lo lote la kukutana na waandishi wa habari na wala hana
mpango wa kuzungumzia msimamo wake ndani ya Serikali na Chama Cha
Mapinduzi.
Tunatumia
nafasi hii kuwataka wale wote wenye tabia ya kuvumisha taarifa zisizo
sahihi waache kufanya hivyo kwa kuwa ni kosa kisheria. Tunawaomba
waandishi wa habari kufuata taratibu za kazi na kutafuta taarifa sahihi
kwenye vyombo vinavyotambulika.
Boniphace Makene
Mwandishi wa Habari wa Makamu wa Rais.
Post a Comment