Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Polisi Wavamia Kituo cha Kukusanya Matokeo UKAWA



Polisi jijini Dar  es  Salaam jana usiku walivamia kituo cha kukusanya matokeo ya nchi nzima cha Chadema kilichopo Kijitonyama na kuwakamata watu wote wanaokiendesha.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Tumaini Makene alisema tukio hilo lilitokea saa nne usiku wakati vijana hao wakiendelea kukusanya matokeo hayo.

Alisema kituo hicho kilichokuwa kikiendeshwa na vijana 800 na wengine maelfu waliokuwa mikoani wakituma matokeo, kilianza kazi hiyo jana asubuhi kikilenga kukusanya matokeo yote, kuyajumlisha na kujua mshindi kabla ya matokeo ya jumla ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

“Kituo chetu kinafanya kazi ile ile kama inayofanywa na kituo cha CCM kilichopo maeneo ya Mlimani City, tunashangaa polisi kuwakamata watu wetu,” alisema Makene.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alisema kwa sasa polisi wanafanya operesheni nyingi na watu mbalimbali wanakamatwa, hivyo asingeweza kujua kama watu hao pia wamekamatwa katika operesheni hiyo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top