Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAGUFULI NI BALAA .... AWAGUSA MPAKA WAKENYA


KATIKA siku chache zilizopita, rais mpya wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amekuwa ‘akitrend’ kwenye mitandao ya kijamii nchini Kenya, wananchi wengi wazalendo wakionekana kuvutiwa na uchapakazi wake ndani ya wiki kadhaa tangu alipotwaa madaraka.


Rais Magufuli ameonyesha kauli mbiu yake ya ‘HAPA KAZI TU’ ambayo haina tofauti na ‘KUSEMA NA KUTENDA’ yake Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta iliyobadilishwa na wazalendo na kuwa ‘KUSEMA NA KUTEMA’ kutokana na kile kinachorejelewa kama ‘uovu’ unaotekelezwa na serikali yake ikizingatiwa kwamba zimwi la ufisadi limekuwa wimbo mitaani.

Uchapakazi wa Magufuli ambaye ni Rais wa awamu ya tano wa taifa hilo, umetuma ujumbe mzito kwa taifa la Kenya ambalo linakabiliwa na visa vingi vya ufisadi kwenye serikali ya Rais Kenyatta na naibu wake William Ruto.
Katika kipindi cha mwezi mmoja tangu alipotwaa madaraka, Magufuli amefanya  mabadiliko makubwa sana katika uongozi wa serikali aliyoikuta.
Awali ya yote, Magufuli amepiga marufuku safari za nje za mawaziri na kutaka mabalozi wa Tanzania kwenye nchi husika kuiwakilisha serikali yake huko. Kwa hatua hiyo, Magufuli amefanikiwa kupunguza matumizi ya pesa za umma kwa ajili ya safari na hela hizo kuelekezwa kufanya mambo mengine ya kuisaidia jamii.
Rais huyu wa awamu ya tano alipunguza bajeti ya awali ya Tsh250 milioni iliyokuwa imetengewa sherehe zakupongezana kwa wabunge walioshinda uchaguzi hadi kufikia Tsh15 milioni.
Fedha zilizobakia zilitumwa kuboresha mahitaji ya hospitali kuu ya kitaifa Muhimbili kwa kununu zaidi ya vitanda 300.
Hii ilikuwa ni baada ya Rais huyo kufanya ziara ya kushtukiza hospitalini humo ambapo aliwakuta wagonjwa wakilala chini kutokana na ukosefu wa vitanda.
Aidha aliifuta bodi ya wakurugenzi wa hospitali hiyo kwa utendakazi duni akiwemo aliyekuwa daktari mkuu Dkt Hussein Kidanto.
Siku chache zilizopita, Magufuli alipunguza ujumbe wa wajumbe 34 waliotakiwa kusafiri nje ya nchi kuiwakilisha Tanzania kwenye kongamano muhimu la kimaendeleo hadi kufikia watu wanne.
Hatua yaokoa donge nono
Hatua hiyo iliokoa Tsh700 milioni ambazo zingetumiwa na wajumbe hao kugharamia safari hiyo.
Jumatatu wiki hii, Magufuli alitangaza kuondoa sherehe za maadhimisho ya siku ya Uhuru inayosherehekewa Desemba 9, na kutaka fedha kwenye bajeti hiyo ya Wakati Wa sherehe hiyo zitumike kwa mambo mengine muhimu.
Haya yakiwa tu ndio baadhi ya vitu alivyovifanya, Wakenya wamepagawishwa naye na kumpelekea kuwa gumzo mitandaoni na kuonekana ‘Top in Town’:

@Fifi: Uhuru Kenyatta anahitaji kujifunza mawili matatu kutoka kwa mwenzake wa Tanzania Magufuli.
@Shadie: Yaani aliyofanya Magufuli ofisini chini ya mwezi mmoja tangu aingie madarakani, yanazidi aliyofanya Uhuru kwa muda wa miaka miwli na nusu tangu awe ofisini.
@MafisiPope: Wakati Magufuli akiwa kwenye hali za kuchapa kazi kwa vitendo wakati ndio siku yake ya pili ofisini, kwa Uhuru imepita miaka mitatu lakini bado yupo ‘bizi’ akiunda kamati akitaka zimweleze cha kufanya.
@Collins Fabien: Rais Uhuru amekuwa akipiga domo tangu 2013 wakati Rais Magufuli amekuwa akichapa kazi kwa wiki tatu sasa.
@Muthui: Wakati Watanzania wakiamka kuyakuta makubwa aliyoyafanya Magufuli, Wakenye tunaamka kuyakuta yale aliyoahidi Uhuru.

Haya yakiwa ni baadhi tu ya maoni ya Wakenya kipindi hiki serikali ya Jubilee inakumbwa na kashfa za kila aina za ufisadi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top