Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MASKINI WEE!! .... MSANII KAJALA APATA PIGO


Staa mwenye mvuto ndani ya Bongo Muvi, Kajala Masanja.
POLE! Staa mwenye mvuto ndani ya Bongo Muvi, Kajala Masanja hivi karibuni alipata pigo zito baada ya kufiwa na bibi yake (mzaa mama) aliyekuwa akiuugua kwa muda mrefu huko mkoani Songea.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda akiwa msibani, Kajala alisema amempoteza mtu muhimu katika maisha yake kwani bibi yake huyo alikuwa akimpenda, kumlea na kumshauri mambo muhimu kwenye maisha.

Kajala alifunguka kuwa alipopata taarifa za msiba wa bibi yake alihisi kuchangayikiwa na maumivu yaliyosababisha mapigo ya moyo kupanda (presha).

“Siwezi kueleza ni jinsi gani nilikuwa nikimpenda bibi yangu, alikuwa ni msaada mkubwa sana kwangu. 

Kila nilipotatizika na jambo lolote sikusita kumfuata na kumshirikisha, kiukweli ni pigo kubwa sana kwangu,” alisema Kajala.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top