Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam imewakamata majambazi saba ndani ya wiki moja waliofanya matukio mbalimbali ya ujambazi Jijini humo.
Akiongea leo jijini Dar es salaam Kamishna wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Simon Sirro amesema kuwa katika oparesheni hiyo pia walifanikiwa kukamata lita 60 za Gongo, silaha aina ya SMG pamoja na bastola zilizokuwa zikitumiwa na majambazi, bangi kete 250, puli 110 pamoja na watuhumiwa wengine 130 kwa makosa mbalimbali.
Kamishna Sirro ameeleza pia kuwa wamefanikiwa kumkamata mwanamke mmoja anayetuhumiwa kwa makosa ya kuwaangalia wateja wanaotoka na fedha benki na kutoa taarifa ili wavamiwe na kunyanga'anywa fedha zao.
Post a Comment