Loading...
TAARIFA MUHIMU YA SASA TOKA IKULU
TAARIFA MUHIMU!!!!!!!!
Karibuni katika matangazo ya moja kwa moja (Live!!!) ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anatunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya 194 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu, vilivyopo katika geti kuu la Mashariki, kandokando mwa Bahari Jijini Dar es Salaam. Matangazo haya yanarushwa Live hii leo kupitia TBC1, TBC Taifa, Azam TV, ITV, Times FM na nyinginezo kuanzia saa Nne kamili asubuhi hii. Kamisheni hii inatolewa kwa mara ya kwanza ndani ya Ikulu, na pia nje ya Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli Mkoani Arusha tangu kihamishwe kutoka Dar es Salaam kwenda Arusha mwaka 1976.
Nyote mnakaribishwa.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais.
Ikulu.
Dar es Salaam
26 Novemba, 2016
Post a Comment