Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kigogo ALAT atumbuliwa kwa ufisadi wa Milioni 90

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini ALAT Bwana Gulam Mukadam.
 *****
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini ALAT Bwana Gulam Mukadam amemsimamisha kazi Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo Bw Abraham Shemoboyo kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa shilingi milioni 150 za ufadhili wa jumuiya hiyo mwaka 2015.

Akiongea katika ofisi za jumuiya hiyo Jijini Dar es salaam, Gulam ambaye pia ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga amesema, benki ya NMB ilitoa kiasi hicho cha pesa kwa jumuiya hiyo kwaajili ya ufadhili wa Tuzo ya Meya (Mayor Awards) na kwamba Katibu huyo  hakuwasilisha kiasi chote na badala yake aliwasilisha shilingi milioni 60 huku kiasi cha shilingi milioni 90 kikiwa hakijulikani kilipo.

Mukadam amesema, uamuzi wa kumsimamisha uliamuliwa na kamati tendaji ya ALAT Taifa na mkutano mkuu wa ALAT taifa, ambapo iliundwa tume ndogo kuchunguza upotevu wa kiasi hicho cha pesa na kuamuliwa kuwa apishe uchunguzi dhidi yake kwa upotevu wa pesa hizo.

Aidha Mstahiki Mukadam amesema, uchunguzi dhidi yake utafanywa na CAG na kwamba pesa hizo hazikuwekwa kwenye akaunt ya ALAT na badala yake zilihifadhiwa kwenye akaunti binafsi ijulikanayo kama 'Vision Investment'.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top