Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Madereva wa Serikali kulipwa sawa na mtu kwenye Elimu ya digrii


Serikali imewaahidi madereva wake kuwa katika bajeti ijayo ya fedha ya 2017/2018, itatekeleza muundo mpya wa ngazi ya mshahara kwa madereva hao, ambapo sasa watakuwa wakipata kiwango cha mshahara sawa na mfanyakazi wa shahada ya kwanza.

Ahadi hiyo imetolewa mjini Dodoma na waziri wa nchi ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bibi Angela Kairuki, katika hotuba iliyosomwa na Afisa Tawala Mkuu katika wizara hiyo ya Utumishi wa Umma, Bw. Wilson Nyamanga.

Hata hivyo Afisa Tawala huyo amewataka madereva wa serikali kutimiza wajibu wao, kwa kuhakikisha suala la nidhamu linapewa kipaumbele wakati wa utekelezaji wa majukumu yao.

Mapema katika risala yao, iliyosomwa na mmoja wa madereva wa serikali Bibi. Anna Mary Kaduma, madereva hao wameishauri serikali kulitafutia ufumbuzi tatizo la matumizi mabaya ya magari, linalofanywa na Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri mbalimbali, na hivyo kuwafanya madereva kufanya kazi katika muda wa ziada, bila ya malipo yoyote.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top