Kamati ya watu 4 yachaguliwa kusimamia mali za marehemu Ivan Ssemwanga mpaka watoto wake watakapofikisha miaka 18. Zari Hassan yumo.
Wengine waliochaguliwa ni Ritah Ssemwanga(Dada wa Ivan), Lawrence Muyanja(Maarufu kama King Lawrence) na George Ssemwanga ambae ni kaka mkubwa wa Ivan.
Zari ametakiwa kusimamia shule za Ivan zilizoko Afrika Kusini kikiwemo chuo cha Brooklyn na pia nyumba mbili za Ivan zilizoko Sandton na Pretoria.
Zari pia ametakiwa aishi na watoto wake wote kwenye nyumba moja na nyingine ipangishwe.
Watu 67 Wauawa Katika Shambulizi Sudan
3 hours ago
Post a Comment