Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS WA ZIMBABWE EMMERSON MNANGAGWA ALIVYOWASILI NCHINI NA KUPOKEWA NA MWENYEJI WAKE RAIS MAGUFULI

1

2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na mgeni wake Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa wakati nyimbo za mataifa mawili ya Tanzania na Zimbabwe zikipigwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara baada ya Rais huyo wa Zimbabwe kuwasili nchini.
3
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku mbili.
4
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akipunga mkono kwa wananchi waliofika katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara baada ya kuwasili nchini kwa ajili ya ziara ya kazi ya siku mbili.
5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha pamoja na  Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
7
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa wakati wakiangalia vikundi mbalimbali vya ngoma za asili katika katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
8
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika mkutano wa Waandishi wa Habari Ikulu jijini Dar es Salaam.
9

10
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akizungumza katika mkutano wa Waandishi wa Habari Ikulu jijini Dar es Salaam. 
6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa mara baada ya kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.PICHA NA IKULU
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top