Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KESI YA LULU KUSIKILIZWA TENA DESEMBA 3

 



MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imeahirisha leo kesi inayomkabili msanii wa filamu Elizabeth Michael Kimemeta (18), maarufu kama Lulu ya mauaji ya msanii mwenzake Steven Kanumba (28) baada ya upande wa Jamhuri kudai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Hata hivyo, wakili wa utetezi Peter Kibatala aliomba mahakama kuhimiza upande wa mashtaka kuongeza kasi ya upelelezi kwa kuwa mshtakiwa anateseka mahabusu.

Hakimu Mkazi Augustina Mmbando alisema upande wa Jamhuri ukamilishe upelelezi na kesi hiyo itatajwa Desemba 3 mwaka huu.
Katika kesi hiyo, Lulu anadaiwa kuwa Aprili 7, mwaka Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam, alimuua Kanumba.

Aidha, kwa mujibu wa Mwenendo wa Sheria ya Makosa ya Jinai (CPA), Lulu hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji lakini mara upelelezi wake utakapokamilika itahamishiwa Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top