Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA MRADI WA UJENZI WA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU MKOANI KATAVI


 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa, wakati alipofika katika Kijiji cha Ilembo Mkoa wa Katavi, Nov 24, kwa ajili ya kuzindua rasmi Ujenzi wa Nyumba za gharama nafuu, zinazojengwa na Shirika hilo, ambapo jumla ya nyumba 250, zinatarajia kujengwa katika eneo hilo. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nehemiah Kyando Mchechu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Nyumba za Gharama nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa, NHC katika Kijiji cha Ilembo Mkoani Katavi. Uzinduzi huo ulifanyika Nov 24, 2012 katika kijiji hicho. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nehemiah Kyando Mchechu (wa pili kulia) ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye na (kushoto) ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dkt. Rajab Lutengwe.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, mkewe Mama Zakhia Bilal (wa pili kushoto) na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye (wa pili kulia) wakikagua sehemu ya ujenzi wa nyumba hizo bada ya uzinduzi wa mpango wa Ujenzi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC, katika kijiji cha Ilembo Mkoani Katavi Nov 24, 2012
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Bilal, akitoka kukagua ujenzi wa njyumba hizo za gharama nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC katika Kijiji cha Ilembo Mkoani Katavi, Nov 24, 2012.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top