Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NIKO TAYARI KIAKILI NA KIMWILI KULITUMIKIA TAIFA: KINANA


KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amewahakikishia Watanzania, hususan wanachama wana-CCM kwamba yupo tayari kimwili na kiakili kuhakikisha anatekeleza kwa ufanisi mkubwa majukumun makubwa aliyopewa kulitumikia taifa.
Kinana alisema hayo leo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Rukwa akiwa katika siku yake ya pili ya ziara ya siku nne katika mikoa ya Mtwara, Rukwa, Geita na Arusha aliyoianza jana.
“Ni kweli nilikuwa nimetangaza kustaafu siasa kwa kuzingatia kwamaba nimeshashika kwa muda mrefu nyadhifa za kuchaguliwa, nikaona kwamba kama wenzako wameshakuamini mwa muda mrefu ukafanya nao kazi wakikupenda, basi usisubiri mapaka uchokwe ndiyo uondoke”, alisema Kinana na kuongeza;
“Lakini sasa baada ya maamuzi yangu, Mwenyekiti wa Chama Chetu, Rais Jakaya Kikwete akaamua kwa kadiri alivyoona inafaa, akaniteua nikisaidie Chama. Kwa mtu mwenye hekima na uadilifu unapoteuliwa na Mwenyekiti wa Chama chako tena Rais wa Chama kinachotawala, lazima ukubali tena bila kinyongo, nikakubali”.
“Sasa baada ya kuwa mimi ndiye Katibu Mkuu wa Chama hiki, napenda kuwaambia kwa dhadi ya moyo wangu kwamba nipo tayari, kimwili, kiakili kuhakikisha nawatumikia Wana-CCM na watanzania kwa jumla kwa weledi na ufanisi mkubwa”.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top