Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SAKATA LAN SHILOLE: ALIEZAA NAE AELEZEA KISA KIZIMA CHA MAISHA YAO


Picha ya shilole na makala enzi hizo


TAARIFA mbalimbali zilizowahi kutolewa na mwigizaji na mwanamuziki maarufu nchini, Zuwena Mohamed 'Shilole' kuhusu uhalisia wa maisha yake zimeelezwa kuwa si za kweli, kwa mujibu wa watu wa karibu na staa huyo.

Shilole aliwahi kuliambia Mwanaspoti Toleo la Septemba 22 mwaka huu lililofanya naye mahojiano kuwa mtoto wake wa kwanza mwenye umri wa miaka 10 alijifungua baada ya kubakwa na baba wa mtoto huyo ambaye amedai kuwa wawili hao walishaishi kama mke na mume kwenye nyumba ya familia ya mume huko Igunga, Tabora.

"Shilole nilijuana naye tangu mwaka 2000, kwa wakati huo alikuwa amemaliza darasa la saba.

Ukweli ni kwamba wote tulikuwa watoto, mwenzangu hakuwa na uangalizi wa karibu na familia yake kwani alikuwa hana wazazi nami pia nilikuwa sina wazazi bali nilikuwa na dada mmoja tu, tulianza kuishi pamoja katika nyumba ya familia," anaanza kwa kusema Makala Joseph mwanamume aliyezaa na Shilole mtoto wa kwanza.

Anasema licha ya kwamba alimkana, akamkimbia, akamsusia mtoto na baadaye akaja kumwiba kwa siri, lakini bado anampenda na kumsihi kama atarudisha moyo wake yupo tayari kumpokea kama mkewe, kwani bado hajaoa akimsubiri Shilole.

Makala ambaye sasa anaishi Igunga mkoani Tabora akifanya kazi ya utingo, anasema kauli ya staa huyo ina athari kubwa kwa mtoto ambaye sasa bado ni mdogo.

"Unaposema kuwa ulibakwa haileti picha na mtazamo mzuri kwa watu, hata hivyo kwa mtoto pia ina athari kubwa, anakua na itafikia kipindi atataka kujua ukweli wa maisha ya mama yake, atakaposikia mama yake alibakwa italeta picha gani?

"Tulikubaliana mpaka tukaishi miaka miwili na kuzaa mtoto ambaye mwenzangu alikimbia na kuniachia mtoto akiwa na miezi mitano mara baada ya kukutana na dereva wa magari makubwa na si kwamba nilimbaka, kama ni hivyo kwanini asingeenda mahakamani na kufungua kesi?" Alihoji Makala.

Anasema ingawa anamtunzia mtoto wake, si vema kwa Shilole kuzungumza kauli zisizo za kweli na kuficha ukweli, huku akiwapakazia watu wengine kesi zisizo kweli.

"Leo ananiona mimi mshamba. Sawa lakini akumbuke kuwa alitoka huku ni vema kuheshimu sehemu uliyotoka kuliko kuleta dharau.

Mimi si msemaji ila tu nimechoshwa na kauli zake, kila siku kwenye magazeti eti alibakwa huku mtuhumiwa nipo kwanini asingeshtaki, hakuna asiyejua hapa Igunga kama niliishi naye kama mke wangu.

"Wakati huo mimi nilikuwa utingo na yeye alikuwa akiuza nyanya sokoni.

Maisha yaliendelea hivyo mpaka alipokuja kupata ujauzito na baadaye alijifungua.

Ila nyongo ilitumbukia baada ya yeye kukutana na huyo bwana ambaye alimshawishi akimbie kwangu na akaenda kumzalisha huko Dar es Salaam."

Kauli ya Makala inafafanuliwa zaidi na dada yake Sara Joseph ambaye ndiye wifi wa Shilole: "Ni kweli yeye hana wazazi kama anavyoeleza katika mahojiano yake kwenye magazeti, redioni na runinga.

Lakini kuna baadhi ya mambo anayoyasema si ya kweli. Angezungumzia maisha yake halisi mimi sina neno, adanganye anavyotaka, lakini si hilo la kuhusu mtoto.

"Kila mtu anajua ipo siku mtoto atakuwa katika hali mbaya na atakuja kutulaumu sisi, kama ameshindwa kulea mtoto atuletee na si kusema alibakwa haileti picha nzuri kwa familia yetu."

Sara ambaye sasa anaishi jijini Dar es Salaam anaeleza namna alivyoilea familia hiyo wakati akiishi Igunga.

"Nilimpokea Shilole akiwa mdogo sana, wakati huo alikuwa akiishi kwa bibi Tatu ambaye ni ndugu wa mama yake aliyeishi na kaka zake wengine wawili Kajiwe na Pascal.

Alikuja na kuanza kuishi na mdogo wangu, kwa kuwa nilikuwa mkubwa nilichukua jukumu la kuwalea wote.

Hii ina maana kuwa hajawahi kusoma sekondari kama anavyodai bali alizaa na mdogo wangu baada ya kuishi naye kwa miaka miwili.

"Ugomvi ulianza kwa kuwa Shilole alikuwa anapenda starehe kuliko mtoto, alitaka kumwacha mtoto na kumfuata mumewe kwenye starehe wakawa wanabishana kila siku mpaka alipokutana na dereva wa magari makubwa akatoroka na kuniachia mtoto akiwa na miezi mitano.

Niliitwa na mtu na kuambiwa kamchukue shangazi yako kajinyea ndipo nilipomkuta mtoto ametelekezwa na yeye amekimbia na bwana," anasema Sara.

Anasema Shilole alirudi Igunga wakati mtoto wake akiwa na umri wa miaka sita. "Nilimlea mtoto mpaka alipotimiza miaka sita, alirudi Igunga na kumchukua mpaka mwaka jana alipomleta kunisalimia wakati wa likizo akiwa na miaka tisa," anasema.

Hata hivyo, wifi wa Shilole anasema baada ya kumpigia akimtaka ajibu tuhuma za kubakwa alijibu: "Nimeandika habari zangu za maisha yangu." Kauli iliyozidi kumfanya ahisi itamharibu mtoto atakapokuwa mkubwa.

Mwanaspoti lilipomtafuta Shilole atoe kauli yake kuhusu suala hilo alisema: "Sina la kujibu kuhusu hilo kwa kweli na kwa sasa nipo bize sana kwani nipo katika matayarisho ya filamu mpya hapa."

SOURCE:http://mwanaspoti.co.tz/
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top