Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ZANZIBAR KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA APPRM


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala bora Haji Omar Kheir (katikati) akiwa katika Kikao ambacho kinajadili Mkutano wa Jumuia ya Afrika ya Utumishi wa Umma na Uongozi (AAPAM) utakao fanyika Zanzibar kuanzia tarehe 12-16 Novemba huko Zanzibar Beach Resort.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala bora Haji Omar Kheir (kulia) akielezea kitu katika Kikao ambacho kinajadili Mkutano wa Jumuia ya Afrika ya Utumishi wa Umma na Uongozi (AAPAM) utakao fanyika Zanzibar kuanzia tarehe 12-16 Novemba huko Zanzibar Beach Resort.


Na Maelezo Zanzibar 01/11/2012


Zanzibar inatarajiwa kuwa Mwenyeji wa Mkutano wa 34 wa Jumuiya ya Kiafrika ya Utumishi wa Umma na Uongozi (AAPAM) utakaofanyika kuanzia Tarehe 12-16 mwezi huu huko katika Ukumbi wa Zanzibar Beach Resort nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa Habari Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haji Omar Kheri huko Ofisini kwake Vuga leo amesema kuwa Mkutano huo uatasaidia katika kuitangaza Zanzibar nje ya Nchi.

Amesema kuwa kutangazwa huko kutasaidia zaidi katika kuimarisha utalii wake ambao unasaidia sana katika uchumi wa Zanzibar ambapo asilimia 80 ya fedha za kigeni zinapatikana kutoka sekta hiyo.

Mbali ya hivyo wajasiriali wa Zanzibar nao kwa upande wao watapata fursa ya kutangaza bidhaa zao kutokana na idadi kubwa ya washiriki kutoka sehemu mbali mbali za nchi za Kiafrika na Jumuiya ya Madola.

Amesema kuwa zadi ya Wajumbe 400 kutoka nchi Jumuiya Wanachama wanatarajiwa kushiriki Mkutano huo ambapo watatafakari juu ya mwenendo wa Utumishi unavyokwenda katika Taasisi mbali mbali Afrika na Duniani.

Akielezea juu ya malengo makuu ya Mkutano huo Waziri Kheri amesema kuwa ni kubadilishana uzoefu katika masuala ya kiutumishi wa Umma na utawala pamoja na kuandaa mipango ya kukabiliana na changamoto zinazoikumba Sekta ya Utumishi wa Umma na Uongozi.

Amewataka Wananchi kujipanga vyema kuutumia Mkutano huo kama fursa nzuri ya kujifunza ili kupata maendeleo ya baadaye na kutoa kila aina ya mashirikiano ya kufanikisha Mkutano huo.

Aidha Waziri Kheri amewata wananchi pia kudumisha usalama ili wageni ambao watashiri katika Mkutano huo kufanya shughuli zao bila ya vikwazo na bughudha yoyote ile.

Mkutano kama huo mwaka jana ulifanyika Nchini Malawi ambapo Mwaka huu hapa Zanzibar Mkutano huo unatarajiwa kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top