Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ajali Tanangozi, Iringa, yauwa wanne papo hapo leo

 




GARI LILILOPATA AJALI TOYOTA RAV 4 T 770 BMP ENEO LA TANANGOZI -IRINGA LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA BWANA EZEKIEL MWAITELEKE (MAREHEMU) MAJIRA YA SAA SITA NA NUSU MCHANA NA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WATANO WA FAMILIA MOJA PAPO HAPO DESEMBA 4, 2012
BAADHI YA AKINA MAMA WASAMARIA WEMA WA TANANGOZI IRINGA WAKIJARIBU KUMPEPELEKA MMOJA WA MAJERUHI WA AJALI ILIYOTOKEA DESEMBA 4,2012 HUKO TANANGOZI IRINGA LIKIHUSISHA TOYOTA RAV 4 T 770 BMP LILILOINGIA NYUMA YA TRAILER T 566 BNQ AMBAPO WATU WATANO WA FAMILIA MOJA WALIOKUWA WAKITOKEA DAR KWENDA MBEYA WALIFARIKI PAPO HAPO
6:BAADHI YA WASAMARIA WEMA WAKITOA MOJA YA MAITI KUTOKA KATIKA GARI TOYOTA RAV 4 T 770 BMP HUKO TANANGOZI IRINGA DESEMBA 4,2012 WATU WATANO WA FAMILIA MOJA WALIOKUWEMO KATIKA GARI HILO WALIFARIKI PAPO HAPO(PICHA ZOTE NA MISANJO LIVIGHA (MLALAHOI ALWATAN WWW.FRANCISGODWIN.BLOGSPOT.COM
GARI AINA YA SCANIA LENYE CABIN NA. T 840 BST LIKIWA NA TRAILER NAMBA T 566 BNQ LILIGONGWA KWA NYUMA NA TOYOTA RAV 4 T 770 BMP HUKO TANANGOZI IRINGA NA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WA TANO WA FAMILIA MOJA PAPO HAPO WALIOKUWA KATIKA GARI HILO RAV 4
Na Francis Godwin
Ajali mbaya imetokea mkoani Iringa mchana wa leo na kusababisha vifo vya watu wanne wa familia moja pamoja na mfanyakazi wa ndani.

Ajali hiyo imetokea katika eneo la Tanangozi wilaya ya Iringa kwenye kizuizi cha barabara cha mafundi wa kutengeneza barabara kuu ya Iringa -Mafinga mkoani Iringa mida ya saa nane mchana

Kwa mujibu wa mashuda wa tukio hilo chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari dogo aina ya Rav 4 lenye namba za usajili T 770 BMP kulipalamia lori lenye tela kwa nyuma. Huku chanzo kikitajwa kuwa ni kuendesha kwa mwendo kasi wa dereva wa gari ndogo marehemu Ezekiel Mwaiteleke na kushindwa kulimudu na kulipalamia lori kwa nyuma.
Kwa mujibu wa mashuda wa tukio hilo chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari dogo aina ya Rav 4 kuendesha kwa mwendo kasi na kushindwa kulimudu na kulipalamia lori kwa nyuma na kuwa gari hiyo ilikuwa ikitokea jijini Dar es Salaam kwenda Kyela mkoani Mbeya.

Hivyo katika ajali hiyo abiria wote wanne akiwemo baba na mama wa watoto wawili waliokuwemo katika gari hiyo pamoja na watoto hao kufa papo hapo na maiti zote kupelekwa katika Hospitali ya mkoa wa Iringa.

Majina ya waliokufa ni pamoja na Ezekiel Mwaiteleke ambaye ni dereva wa gari hilo na baba wa familia hiyo ,mkewe Grace Mwaiteleke ,mtoto Kelvin Mwaiteleke (2),Happy Mwandike na mfanyakazi wao wa ndani aliyefahamika kwa jina la Linda Ezekiel huku majeruhi katika ajali hiyo ni mmoja na amekimbizwa Hospital ya mkoa wa Iringa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top