Askofu Msaidi wa Jimbo Kuu la 
Dar es Salaam,  Eusebius Nzigilwa  (katikati) akiongoza ibada ya mkesha wa Sikuu 
ya Krismasi katika Kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es Salaam 
juzi. Kushoto ni Paroko wa kanisa hilo, Padri, Joseph Mosha.  (Picha na Habari 
Mseto Blog)
 Askofu Mkuu wa Kanisa la 
Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa akitoa mahubiri wakati 
wa ibada ya Krismasi leo.
 Askofu Mkuu wa Kanisa la 
Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa akitoa baraka kwa 
waumini wa Usharika wa Azania Front baada ya ibada ya Krismasi
Sehemu ya waumini wa Kanisa 
Katoliki Parokia mpya ya Mt. Bonaventure, Kinyerezi wakifuatilia sehemu ya ibada 
ya Krisamsi iliyokuwa ikiendeshwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, 
Muadhama Polycarp Kadinali Pengo, Dar es Salaam leo.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la 
Dar es salaam Muadhama Polycarp Kadinali Pengo akipokea michango mbalimbali ya 
fedha kutoka kwa viongozi wa jumuiya za kikristo katika jimbo la segerea, dar es 
salaam alipokwenda kuongoza ibada ya Krismasi sambamba na uzinduzi wa Kanisa 
Katoliki Parokia ya Mt. Bonaventure, Kinyerezi, Dar es Salaam leo.




Post a Comment