Marehemu Eustace Nyaruganda
WANAHARAKATI wa
waangaliza wa haki za binadamu kutoka nchi mbali mbali za Afrika Mashariki ambao
wanaendelea na mafunzo ya uangalizi wa haki za binadamu jijini Daresalaam
wameeleza kusikitishwa na taarifa za kifo cha mwanaharakati mwenzao haki za
binadamu wa mkoa wa Mara Eustace Nyaruganda 45 aliyekutwa amekufa katika nyumba
moja ya kulala wageni(Guest) mjini hapo.
Mbali ya kusikitishwa na
mauwaji ya mwanaharakati mwezao huyo pia wameeleza kusikitishwa na kitendo cha
kinyama alichotendewa mwandishi wa habari wa magazeti ya Free Media Shaban
Matutu aliyepigwa risasi na watu wanaosadikika kuwa ni askari polisi matukio
waliyodai kuwa ni kinyume na haki za binadamu .
Wakizungumza leo katika
mahojiano maalum na kipindi cha gali la matangazo la Radio Nuru Fm ya mkoani
Iringa kutoka Hotel ya White Sands Kunduji jijini hapa wanaharakati hao akiwemo
mwanaharakati aliyekuwa akifanya kazi na marehemu huyo mkoani Mara Angela
Benedict na afisa shughuli wa shirika la ABC Foundation,Andreas Migiro walisema
kuwa wamepokea kwa masikitiko makubwa juu ya taarifa za msiba wa mkurugenzi wake
aliyekuwa amekufa asubuhi ya leo ikiwa ni baada ya kupotea katika mazingira ya
kutatanisha kwa siku kadhaa .
Wakati Angela akidai
kuwa taarifa ya kifo hicho imemshitua
zaidi na kuomba uchunguzi wa kina wa kifo cha mwenzao huyo kutolewa bado kwa
upande wake Migiro alisema kuwa alipewa taarifa kuwa mkurugenzi wao alikutwajana
asubuhi akiwa amekufa katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la
Savana iliyoko katika mtaa wabenki mjini Bunda.
Akizungumzia kifo hicho
cha mwanaharakati huyo,mratibu wa mtandao wa kutetea watetezi wa haki za
binadamu nchini,Tanzania Human Right Defenders Coalitions, Onesmo ole Ngulumwa
amesema kuwa mtandao umepokea kwa masikitiko makubwa sana juu ya kifo hicho na
kwamba ni pigo kwa watetezi wa haki za binadamu kwani alimfahamu kwa karibu sana
marehemu na kuwa kituo chake kitatoa taarifa kamili juu ya kifo hicho mapema leo
.
Mratibu huyo alisema
kuwa anatarajia leo kuongea na vyombo vya habari juu ya tukio la kifo hicho cha
mwanaharakati ambapo pia amewaomba ndugu na jamaa wa karibu na marehemu ikiwa ni
pamoja na jeshi la polisi kuhakikisha wanasimamia kwa karibu ili mwili wake
uweze kufanyiwa uchunguzi wa kina na dakitari kabla haujazikwa.
Hata hivyo baadhi ya
wanaharakati wanaohudhilia mafunzo hayo wameonyesha kusikitishwa sana na
mazingira ya kifo hicho ambapo wamesema kuwa hivi sasa maisha ya wanaharakati
yako hatalini hivyo ni lazima waishi kwa tahadhali sana.
Kamanda wa polisi mkoa
wa Mara Absalum Mwakyoma alipopigiwa simu alisema hana taarifa na tukio hilo na
akasema apigiwe simu mkuu wa polisi wa wilaya hiyo ambapo yeye pia alisema yuko
safari na kuelekeza kwa mkuu wa upelelezi wa wilaya ambaye alithibitisha kutokea
kwa tukio hilo na kwamba wanaendelea na upelelezi zaidi.
Wakati huo huo
mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini Tanzania Absalom Kibanda akieleza
kusikitishwa na vitendo vya uvunjifu wa amani vinavyoendelea kufanywa na jeshi
la polisi nchini na kuwa itafika wakati wanahabari nchini watahofia kufanya kazi
na jeshi la polisi kutokana na vitendo hivyo vinavyoendelea kufanyiaka na kuona
kama polisi ni maja ya maeneo ya hatari kwa wanahabari nchini .
Kibanda alidai kuwa
anashindwa kujua sababu ya jeshi la polisi kumpiga risasi mwandishi wa gazeti la
Tanzania daima Bw Matutu akiwa nyumbani kwake na kudai kuwa tukio hilo
limefanyika kwa bahati mbaya na kuwa wao walikuwa wakimsaka mtuhumiwa wao wa
kike na badala yake kumpiga mwanahabari huyo.
Marehemu Eustace Nyaruganda
WANAHARAKATI wa
waangaliza wa haki za binadamu kutoka nchi mbali mbali za Afrika Mashariki ambao
wanaendelea na mafunzo ya uangalizi wa haki za binadamu jijini Daresalaam
wameeleza kusikitishwa na taarifa za kifo cha mwanaharakati mwenzao haki za
binadamu wa mkoa wa Mara Eustace Nyaruganda 45 aliyekutwa amekufa katika nyumba
moja ya kulala wageni(Guest) mjini hapo.
Mbali ya kusikitishwa na
mauwaji ya mwanaharakati mwezao huyo pia wameeleza kusikitishwa na kitendo cha
kinyama alichotendewa mwandishi wa habari wa magazeti ya Free Media Shaban
Matutu aliyepigwa risasi na watu wanaosadikika kuwa ni askari polisi matukio
waliyodai kuwa ni kinyume na haki za binadamu .
Wakizungumza leo katika
mahojiano maalum na kipindi cha gali la matangazo la Radio Nuru Fm ya mkoani
Iringa kutoka Hotel ya White Sands Kunduji jijini hapa wanaharakati hao akiwemo
mwanaharakati aliyekuwa akifanya kazi na marehemu huyo mkoani Mara Angela
Benedict na afisa shughuli wa shirika la ABC Foundation,Andreas Migiro walisema
kuwa wamepokea kwa masikitiko makubwa juu ya taarifa za msiba wa mkurugenzi wake
aliyekuwa amekufa asubuhi ya leo ikiwa ni baada ya kupotea katika mazingira ya
kutatanisha kwa siku kadhaa .
Wakati Angela akidai
kuwa taarifa ya kifo hicho imemshitua
zaidi na kuomba uchunguzi wa kina wa kifo cha mwenzao huyo kutolewa bado kwa
upande wake Migiro alisema kuwa alipewa taarifa kuwa mkurugenzi wao alikutwajana
asubuhi akiwa amekufa katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la
Savana iliyoko katika mtaa wabenki mjini Bunda.
Akizungumzia kifo hicho
cha mwanaharakati huyo,mratibu wa mtandao wa kutetea watetezi wa haki za
binadamu nchini,Tanzania Human Right Defenders Coalitions, Onesmo ole Ngulumwa
amesema kuwa mtandao umepokea kwa masikitiko makubwa sana juu ya kifo hicho na
kwamba ni pigo kwa watetezi wa haki za binadamu kwani alimfahamu kwa karibu sana
marehemu na kuwa kituo chake kitatoa taarifa kamili juu ya kifo hicho mapema leo
.
Mratibu huyo alisema
kuwa anatarajia leo kuongea na vyombo vya habari juu ya tukio la kifo hicho cha
mwanaharakati ambapo pia amewaomba ndugu na jamaa wa karibu na marehemu ikiwa ni
pamoja na jeshi la polisi kuhakikisha wanasimamia kwa karibu ili mwili wake
uweze kufanyiwa uchunguzi wa kina na dakitari kabla haujazikwa.
Hata hivyo baadhi ya
wanaharakati wanaohudhilia mafunzo hayo wameonyesha kusikitishwa sana na
mazingira ya kifo hicho ambapo wamesema kuwa hivi sasa maisha ya wanaharakati
yako hatalini hivyo ni lazima waishi kwa tahadhali sana.
Kamanda wa polisi mkoa
wa Mara Absalum Mwakyoma alipopigiwa simu alisema hana taarifa na tukio hilo na
akasema apigiwe simu mkuu wa polisi wa wilaya hiyo ambapo yeye pia alisema yuko
safari na kuelekeza kwa mkuu wa upelelezi wa wilaya ambaye alithibitisha kutokea
kwa tukio hilo na kwamba wanaendelea na upelelezi zaidi.
Wakati huo huo
mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini Tanzania Absalom Kibanda akieleza
kusikitishwa na vitendo vya uvunjifu wa amani vinavyoendelea kufanywa na jeshi
la polisi nchini na kuwa itafika wakati wanahabari nchini watahofia kufanya kazi
na jeshi la polisi kutokana na vitendo hivyo vinavyoendelea kufanyiaka na kuona
kama polisi ni maja ya maeneo ya hatari kwa wanahabari nchini .
Kibanda alidai kuwa
anashindwa kujua sababu ya jeshi la polisi kumpiga risasi mwandishi wa gazeti la
Tanzania daima Bw Matutu akiwa nyumbani kwake na kudai kuwa tukio hilo
limefanyika kwa bahati mbaya na kuwa wao walikuwa wakimsaka mtuhumiwa wao wa
kike na badala yake kumpiga mwanahabari huyo.
Post a Comment