Mkuu wa Bandari ya Kigoma,
Bw. Sebastian Nandi akimuonyesha eneo la Bandari ya Kasanga, Naibu Waziri wa
Uchukuzi, Dkt. Charles Tizeba(aliyevaa suti ya kaki), leo asubuhi. Naibu Waziri
wa Uchukuzi yuko Mkoani Rukwa kwa ziara ya kuangalia shughuli mbalimbali
zinazofanywa na taasisi zilizo chini ya Wizara ya
Uchukuzi.
Naibu Waziri wa
Uchukuzi,Dkt Charles Tizeba(aliyevaa suti ya kaki), akisisitiza jambo kwa
Uongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA), alipotembelea Bandari ya Kasanga
Mkoani Sumbawanga leo asubuhi.
Naibu Waziri wa Uchukuzi,
Dkt Charles Tizeba(aliyevaa suti ya kaki), akiangalia mzigo wa Saruji,
uliohifadhiwa kwenye magodauni ya Mamlaka ya Bandari ya Kasanga, alipotembelea
bandari hiyo leo asubuhi.
Naibu Waziri wa
Uchukuzi,Dkt Charles Tizeba (aliyevaa suti ya kaki ),akiangalia maporomoko ya
Kalambo yaliyoko Mkoani Rukwa leo asubuhi. Maporomoko hayo ni ya pili kwa ukubwa
barani Afrika, ya kwanza yakiwa yale ya Viktoria Falls yaliyoko
Zimbabwe.
Naibu Waziri wa Uchukuzi,
Dkt Charles Tizeba(aliyevaa suti ya kaki), akibadilishana mawazo na Mtendaji wa
kijiji cha Kapozwa Sumbawanga, Bw. Abeid Mwanakatwe (aliyevaa flana ya rangi ya
Maziwa)mara baada ya kuangalia maporomoko ya Kalambo leo
mchana.
Kaimu Mkurugenzi wa
Uhandisi na Ufundi wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege(TAA), Mhandisi George
Sambali, akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dkt Charles
Tizeba(aliyevaa suti ya kaki),ya namna ambavyo Uwanja wa Ndege Mpya Unaotaka
kujengwa katika eneo la Kisumba mkoani Sumbawanga utakavyokuwa leo
mchana.
Naibu Waziri wa
Uchukuzi,Dkt Charles Tizeba(aliyevaa suti ya kaki),akifafanua jambo kwa uongozi
wa kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga katika ofisi za kiwanja hicho leo
Mchana.
Muonekano wa Kiwanja cha
Ndege cha Sumbawanga. Kwa mwaka 2012 idadi ya abiria imefikia wastani wa 200 kwa
Mwezi ikilinganishwa na miaka ilipita na matarajio kufikia mwishoni mwa mwaka
2012 idadi ya abiria itazidi na kufikia 1,000.
Naibu Waziri wa
Uchukuzi,Dkt Charles Tizeba(aliyevaa suti ya kaki),akisistiza jambo kwa uongozi
wa Kiwanja Cha Ndege Cha Sumbawanga leo Mchana,alipotembelea kiwanja kujionea
namna kinavyofanya kazi.Naibu Waziri ameuagiza uongozi wa kiwanja hicho pamoja
na mambo mengine kuhakikisha wanaweka uzio maana Wananchi wanapita katikati ya
uwanja huo kwa sababu ya kukosa Uzio.
Post a Comment