Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ratiba ya kuadhimisha miaka 49 ya sherehe za mapinduzi hii hapa

Sherehe za miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar zinaanza rasmi hapo Januari, 4 mwezi ujao kwa Wilaya za Unguja na Pemba kufanya usafi wa Mazingira katika maeneo yao.

Kwa mujibu wa Ratiba iliotolewa na Kamati ya sherehe hizo imeonesha kuwa miradi 62 itazinduliwa na mengine kuwekwa jiwe la msingi katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba.

Ratiba hiyo imeonesha kuwa tarehe 5mwezi ujao asubuhi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein atafunguwa Jengo la Chuo cha Utawala wa Umma ,huko Tunguu Wilaya ya kati Unguja Mkoa wa Kusini Unguja.

Jioni Dkt Shein atafunguwa mradi wa E -Government Mazizini Wilaya Magharibi Unguja.


Tarehe hiyo hiyo 5 asubuhi Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad huko Kisiwani Pemba atafunguwa Skuli mpya ya Sekondari ya Wawi iliopo Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba na jioni atafunguwa Maabara katika Hospitali ya Cottage ya Micheweni Mkoa
wa Kaskazini Pemba.

Nae Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd jioni huko Kizimbani Wilaya ya Magharibi Unguja atafunguwa Bweni la Wanafunzi wa Kilimo.

Mnamo tarehe 6 asubuhi huko Maruhubi Wilaya ya Mjini Unguja Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dtk Ali Mohamed Shein atafunguwa Bohari Kuu ya Dawa ambapo jioni siku hiyo Rais Mstaafu Dkt Amani Abeid Karume atafunguwa skuli mpya ya Sekondari huko Muwanda Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskani Unguja.

Mbali na shughuli hizo pia Dkt Shein tarehe 7 atafunguwa Skuli mpya ya Sekondari ya Uzini ilipo Wilaya ya Kati Unguja Mkoa wa Kusini Unguja ambapo jioni huko Nungwi Wilaya ya Kaskazini A Unguja Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt Mohamed Gharib Bilal atafunguwa Hoteli ya Nyota tano.

Kisiwani Pemba siku hiyo jioni Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd Makangale, Wilaya ya Micheweni atafunguwa Hoteli ya Ndani ya Maji,"MANTA REEF RESORT"na asubuhi Wilaya ya Mkoa Michenzani Chokocho atafunguwa Mradi wa Maji Safi na Salama.

Asubuhi ya tarehe 8 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Ali Shein hapo Raha Leo Wilaya ya Mjini Unguja atafanya ufunguzi wa Mradi wa kuhama kutoka Teknologia ya Analojia kwenda Dijitali na ufunguzi wa Studio ya kurikodi sanaa na Muziki.

Asubuhi hiyo hiyo huko Micheweni Pemba Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd atafunguwa kituo cha Afya kiliopo Chimba Wilaya ya Micheweni Pemba ambapo asubuhi hiyo hiyo katika Wilaya ya Kaskazini A, Unguja Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi atafunguwa Skuli mpya ya
Sekondari ya Mapinduzi iliopo Chaani Wilaya ya Kaskazini A.

Jioni katika Wilaya ya Kaskazini B Unguja Dkt Shein atafunguwa Barabara ya Mfenesini hadi Bumbwini ambapo tarehe 9 Wilaya ya Kaskazini A Unguja Makamo wa kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad atafunguwa Skuli ya Msingi iliopo mbuyu Mtende

Tarehe 10 jioni kutakuwapo na ufunguzi wa Mradi wa "One World Football for Africa ambapo Rais wa Zanzibar Dkt Shein atakuwa Mgeni rasmi kwenye Uwanja wa Amani Mjini Zanzibar na asubuhi Balozi Seif Ali Idd huko Dole Wilaya ya Magharibi Unguja atafunguwa Skuli Mpya ya Sekondari ya Mikindani iliopo Dole.

Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd tarehe 11 asubuhi atafunguwa Majengo Mapya ya Nyumba za Wazee Sebleni zilopo Wilaya ya Mjini Unguja na jioni huko Matemwe Wilaya ya Kaskazini A Unguja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho
Kikwete atafungua Skuli mpya ya Sekondari ya Mlimani.


Usiku siku hiyo katika Wilaya ya Mjini Unguja kutakuwa na maonesho ya Ngoma za Utamaduni na Muziki katika Mesi ya Polisi Ziwani na pia kupigwa Mizinga, Kurushwa Fash Fash na Meli ziliopo Bandarini na Gari ziliopo Barabarani zitapiga Honi na Ving'ora.


Tarehe 12 ndio kilele cha Sherehe ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein atakaguwa Gwaride Rasmi la Vikosi vya Ulinzi na Usalama na Vikosi vya Serikali Mapinduzi Zanzibar pamoja na Maandamano ya Wananchi wa Mikoa mitano ya Zanzibar na baadae kulihotubia Taifa huko katika Uwanja wa Amani,

Mbali na Shughuli hizo za uzinduzi wa Miradi mbali mbali zitakazofanywa na Viongozi wa juu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Tanzania, pia Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Muungano watazinduwa na kufunguwa Miradi mbali mbali ukiwamo ule wa
Ufunguzi wa Mnara wa Redio wa Masafa ya Kati ambapo Waziri wa Mawasiliano ,Sayansi na Teknolojia, Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania Prof,Makame Mbarawa atafunguwa na pia kuwekwa jiwe la msingi Skuli ya Moga Wilaya ya Kaskazini A Unguja ambapo Naibu Waziri wa
Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Bihindi Hamad Khamis ataifanya kazi hiyo.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top