
Taarifa hiyo inaonyesha kuwa jumla ya wanafunzi 560,706 kati ya 865,534 waliofanya mtihani wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za sekondari za serikali, ambapo idadi hiyo ni sawa na asilimia 64.78 ya wanafunzi waliofanya mtihani.
Aidha kati ya wanafunzi waliochaguliwa wasichana ni 281,460 sawa na asilimia 50.20 na wavulana ni 279,246 sawa na asilimia 49.80.
Pia takwimu zinaonyesha waliofutiwa matokeo kutokana na vitendo vya udanganyifu katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2012 imepungua sana, kwani ni watahiniwa 293 tu ikilinganishwa na watahiniwa 9,736 waliofutiwa matokeo mwaka 2011.
Post a Comment