Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege la
Turkish Airlines Dkt.Temel Kotl akishuka kwenye ndege ya Turkish Airlines aina
ya B737-900 wakati wa hafla uzinduzi wa safari ya ndege hiyo ya
Instabul-Kilimanjaro iliyofanyika leo kwenye Uwanja wa Ndege wa KIA.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Mngodo (wanne kushoto) akikata utepe kuzindua safari
ya Shrika la Ndege la Turkish Airline kwenye Uwanja wa KIA
jana.
Watatu kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege la Turkish
Airlines Dkt.Temel Kotl.
Baadhi
ya abiria wakishuka akishuka kwenye ndege ya Turkish Airlines aina ya B737-900
wakati wa hafla uzinduzi wa safari ya ndege hiyo ya Instabul-Kilimanjaro
iliyofanyika kwenye Uwanja wa Ndege wa KIA
Mkurugenzi
Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege la Turkish Airlines Dkt.Temel Kotl akikabidhi
zawadi kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KADCO Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Shirika la
Ndege la Turkish Airlines Dkt.Temel Kotl wakati wa hafla uzinduzi wa safari ya
ndege ya Turkish Airlines ya Instabul-Kilimanjaro katika hafla siliyofanyika
kwenye Uwanja wa Ndege wa KIA.
Na
Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Ndege la Turkish
Airlines limeanza rasmi kutumia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro
(KIA) jana kwa safari zake za Instabul-Kilimanjaro – Mombasa kufuatia jitihada
za kuboreshwa na kutangaza uwanja huo zinazofanywa na kampuni inayoendesha
uwanja huo ya Kilimanjaro Airport Development Company (KADCO).
Shirika hilo ambalo litafanya
safari mara tano kwa wiki liaungana na kampuni za ndege nyingine za Qatar
Airways, Qatar ,KLM,Edelweiss Air, Condo Air na Ethiopian Airlines ambayo tayari
yamezindua safari zake kupitia uwanja huo.
Akizungumza wakati wa hafla
ya uzinduzi wa Safari ya Shrika la Ndege la Turkish Airlines kwenye Uwanja wa
Ndege wa KIA jana, Mwenyekiti wa Bodi ya KADCO Balozi Hassan Kibelloh alisema
mvuto wa uwanja huo umetokana na jitihada za makusudi zilizofanya na kampuni
yake ilikuufanya uwanja huo kuwa na muonekano wa kimataifa.
“Tunashukuru kwa ujio wa
ndege hii ya kimataifa ya Turkish Airlines. Ujio ha ndege hii unatupachangamoto
ya kuendelea kuboresha huduma zetu ilituendelee kuvutia ndege nyingine za
kimataifa,” alisema.
“Hi ni ishara kuwa Shirika la
Turkish Airlines lina imani na uwanja wetu na itatoa fursa nzuri kiushindani.
Kutua kwa ndege hii kutaiunganisha Tanzania na nchi nyingine jirani katika
masoko yapatikanayo Marekani, Canada na nchi za Ulaya kupitia mtandao mkubwa wa
Shirika la Ndege la Turkish.
Nae Mkurugenzi Mtendaji Mkuu
wa Shirika la Ndege la Turkish Airlines Dkt.Temel Kotl wakati wa hafla hiyo
alisema kuwa kampuni yake ina imani kubwa na bara la Afrika nakuongeza kuwa
wanatarajia kufungua safari nyingine saba kwenye bara la Afrika siku
zijazo.
“Tuna imani kubwa na soko
liliopo kwenye bara via Afrika na lego letu kubwa kwa sasa ni kuunganisha bara
la Afrika na nchi nyingine zaidi duniani. Kwa kuliangalia hilo, tunategemea
kuaanzisha safari nyingine saba kwenye Bara la Afrika,” alisema.
Naye Balozi wa Uturuki ncini
Ali Davutoglu wakati wa shuguli hiyo alisema nchi yake imesaidia ukuaji wa sekta
mbali mbali Barani Afrika zikiwemo elimu, biashara na kilimo.
“Ushirikiano wetu kibiashara
na Bara la Afrika unakua kwa kasi sana. Mapato kupitia biashara kati ya Tanzania
yamekuwa kutoka dola milioni 18 mwaka 2004 mpaka dola milioni 198 mwishonmi wa
mwaka 2011,” alisema.
Post a Comment