Katika ziara
hiyo iliyodhaminiwa na shirika la hifadhi za taifa nchini (TANAPA), msanii huyo
aliyeambatana na mumewe ambaye ndiye anesimamia kazi zake, Gadna Habash,
waliwasili kwenye lango kuu la Marangu saa
12 jioni na
kupokelewa na mhifadhi mkuu wa hifadhi ya mlima Kilimanjaro (KINAPA), Erastus
Lufungulo.
Akizungumza
kwenye mkutano na waandishi wa habari mara baada ya kushuka mlimani, Jay Dee,
alisema ziara hiyo imetoa mafunzo makubwa kwao na wakatoa wito kwa wasanii,
waandishi wa habari na watangazaji nchini, kutembelea vivutio hivyo ili kufahamu
yale wanayozungumza kuhusu hifadhi hizo.
Kwa upande
wake mhifadhi wa KINAPA Lufungulo ametoa rai kwa wadau wote hasa wananchi wa
kawaida kushiriki kupanda mlima huo, kwa lengo la kukuza utalii wa
ndani.
Post a Comment