Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UMOJA WA VIJANA CCM WAJENGA CHOO IRINGA

 


Na: Denis Mlowe - Iringa
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi mkoani Iringa wanatarajia kujenga choo katika sehemu maarufu zaidi mkoani hapa kwa biashara ya nyama ya nguruwe na vinywaji kama Vibanda vya ccm. Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wa habari hii Rhoda George ambaye Katibu wa Vijana wa chama hicho mkoani hapa amesema kwamba choo hicho
hadi kukamilika kwake kitatumia zaidi ya shilingi milioni 3 kwa ajili ya ujenzi, kununulia vifaa na malipo kwa mafundi.
" Kutokana na sehemu hiyo kuongezeka kwa wateja kila siku tumeamua kujenga choo chenye matundu manne kwa ajili ya wanaume na wanawake ili kuepusha madhara zaidi ya magonjwa yanayoweza kujitokeza kuliko mwanzo" alisema Rhoda

aidha amesema kwamba mara ya baada ya kukamilika watakaa pamoja na wafanyabiashara wa maeneo hayo kwa lengo la kujadili jinsi ya kukiendesha choo hicho kuliko ilivyo sasa vyoo vyote vinakabiliwa na uchafu kutokana na kutokuwa na matunzo jambo linalofanya mamlaka husika kuwafungia mara kwa mara.

Sehemu hiyo ya biashara kulikuwa hakuna vyoo vya kujitosheleza na wateja wengi walikuwa wakijisaidia maeneo ambayo si sahihi.

Naye Naibu Meya wa Manispaa Gervas Ndaki amewapongeza ccm vijana kwa kuweza kufanikisha ujenzi huo kwani ni jambo la heri na kuwataka wateja waweze kukitumia kuzingatia usafi.
"Vijana wanafanya kazi nzuri kutokana na ilani ya ccm hivyo ni jambo la kuwapongeza sana na waangalie maeneo mingine waweze kuboresha huduma hiyo ya vyoo kwa maeneo wanayomiliki" alisema Ndaki

Mmoja wa wamiliki wa mabanda hayo Thedy Ngaita alisema ni jambo zuri kwani wateja walikuwa wanajisaidia maeneo ambayo si sahihi.
"kwa kweli iko poa sana na tunaona ujenzi huu utatukomboa sana kuondokana na magonjwa kama UTI vyoo vilikuwa vichafu sana na ndio chanzo cha kufungiwa biashara zetu mara kwa mara nawapongeza kwa kweli" alisema Ngaita

Mara kwa mara maeneo hayo yanayomilikiwa na umoja wa vijana wa ccm yalikuwa yanafungiwa kutokana na uchafu wa vyoo na mazingira hatari kwa watumiaji na inakadiliwa zaidi ya wafanyabiashara 100 wako maeneo ya mabanda hayo
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top