.

Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA Mabere Marando amesema kundi kubwa la walioshinda kwenye huo uchaguzi halina uwezo kuanzia wajumbe wa halmashauri kuu ya taifa (NEC), wenyeviti pamoja na viongozi wengine wa ngazi ya mkoa, wilaya, kata na vijiji.
Marando amesema hiyo ishu itasababisha CCM ipate wakati mgumu katika chaguzi zijazo, namkariri akisema “matukio ya rushwa na ufisadi yaliyotokea wakati wa uchaguzi mkuu huo, kuna viongozi waandamizi wa CCM ambao wamelalamika hadharani kuhusu kuenguliwa kutokana na rushwa ndani ya CCM, walijidai kwamba hatua zitachukuliwa dhidi ya vitendo hivi na wahusika lakini mpaka leo uchaguzi umekwisha tunajua hakuna hatua iliyochukuliwa dhidi ya mtu yeyote”
Nape Nnauye.

Kwenye sentensi nyingine, Nape amesema “yeye sio wa kwanza, alianza Babu Dr. Slaa akasema Oooh unajua timu ni ile ile, kama yapo maeneo yalikua na malalamiko ya rushwa tumekamilisha juzi, kamati na udhibiti na nidhamu itapitia maeneo machache ambayo yamelalamikiwa”
credits
; Millard Ayo
Post a Comment