Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS KIKWETE KUFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA POLISI

imagesRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Jakaya Mrisho Kikwete leo anatarajiwa kufungua mkutano mkuu wa mwaka wa maofisa wakuu waandamizi wa Polisi mjini Dodoma, utakaowashirikisha makamanda wote wa mikoa na vikosi utakaodumu kwa siku nne.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana Mjini Dodoma, Msemaji wa Jeshi hilo Bi. Advera Senso alisema Lengo la mkutano huo ni kujadili mambo mbalimbali ya kiutendaji ikiwemo utekelezaji wa maazimio yaliyoafikiwa katika mkutano wa mwaka 2012 pamoja na kuweka mikakati ya namna ya kuendelea kudhibiti na kukabiliana na vitendo vya uhalifu hapa nchini.
Bi. Senso alisema katika mkutano huo, mada mbalimbali zitatolewa na wadau kutoka ndani na nje ya Jeshi la Polisi ambazo zitalenga kuimarisha uwezo wa namna ya kuzuia, kupambana na kutanzua uhalifu hapa nchini kuanzia ngazi ya familia.
“Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na mawaziri mbalimbali akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Waziri wa Fedha, Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi, Waziri wa Kazi na Ajira, Waziri wa Maliasili na Utalii, Waziri wa Kilito, Chakula na Ushirika, Waziri wa Ardhi na Makazi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tamisemi, Waziri wa Katiba na Sheria, Waziri wa Mifugo na Uvuvi pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto” Alisema Bi. Senso.
Kauli mbiu katika mkutano huo ni “Tujenge uwezo wa jamii na Polisi kukabiliana na vurugu kwa kuimarisha utii wa sheria bila shuruti
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top