Kundi la
kwanza la Cameroon likiongozwa na kiungo wa zamani wa Toulouse ya Ufaransa
ambaye sasa yuko Al Ahli ya Falme za Kiarabu (UAE), Achille Emana na Meneja wa
timu hiyo Rigobert Song litatua nchini kesho (Februari 3 mwaka huu) saa 4.40
usiku kwa ndege ya KLM.
Wachezaji
wengine katika kundi hilo ni Vincent Aboubakary anayechezea timu ya Valenciennes
iliyoko Ligi Kuu ya Ufaransa, kipa Charles Itandje anayedakia timu ya POAK FC ya
Ugiriki, Kocha wa viungo Sylvain Monkam.
Mshambuliaji
wa Anzhi Makhachkala ya Urusi ambaye ndiye nahodha wa Cameroon, Samuel Eto’o
ataongoza kundi la pili litakalowasili nchini Februari 4 mwaka huu (saa 3.45
asubuhi) kwa ndege ya Kenya Airways kupitia Nairobi, Kenya.
Wengine
katika ndege hiyo Herve Tchami wa Budapest Honved ya Hungary, beki Nicolas
Nkoulou wa Marseille ya Ufaransa, mshambualiji Jean Paul Yontcha wa SC Olhanense
ya Ureno na daktari wa timu Dk. Boubakary Sidik wakati Kocha wa timu hiyo Jean
Paul Akono na msaidizi wake Martin Ndtoungou watawasili saa 4.40 asubuhi kwa
ndege ya Kenya Airways akitokea Afrika Kusini.
Februari
4 mwaka huu kuna kundi lingine litakaloingia saa 4.40 usiku kwa ndege ya KLM
ambalo lina beki Jean Kana Biyick wa Rennes ya Ufaransa, mshambuliaji Fabrice
Olinga wa Malaga FC ya Hispania, beki Allan Nyom wa Udinese ya Italia ambaye
yuko kwa mkopo Granada ya Hispania na beki wa kushoto Henri Bedimo wa
Montpellier ya Ufaransa.
Wachezaji
waliobaki wakiongozwa na kiungo wa Barcelona, Alexandre Song watawasili Februari
5 mwaka huu kwa muda tofauti kwa ndege za KLM na Kenya Airways.



Post a Comment