Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

LOWASSA ALIPUUZWA UJENZI WA MAGHOROFA

GHOROFA LILILOANGUKA JANA
UZEMBE wa serikali kutotekeleza mapendekezo ya ripoti iliyobaini upungufu kwenye majengo marefu ya ghorofa umeleta tena maafa kwa watu watano kupoteza maisha na wengine 15 kujeruhiwa.

Tukio hilo limetokea jana asubuhi baada ya jengo la ghorofa 16 lililokuwa linaendelea kujengwa katika mitaa ya Indira Ghandi na Morogoro kuporomoka na kusababisha taharuki kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo ya katikati ya jiji.

Hata hivyo, huenda idadi ya vifo ikaongezeka kutokana na watu wengine zaidi ya 40 kuhofiwa kufunikwa na kifusi wakiwamo mafundi pamoja na watoto waliokuwa wakicheza jirani na jengo hilo.

Jengo hilo lililoko katika kitalu Na.166 ni mali ya Raza Ndagji na mjenzi wake ni Kampuni ya Lucky Construction Limited.

Baadhi ya watu walidai jengo hilo kujengwa chini ya kiwango kutokana na vifaa vilivyotumika, ingawa mkandarasi huyo hajapatikana kulieleza hilo wakati huu ambapo uokoaji unaendelea kwa kutumia vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama.

Majeruhi hao 15 walipelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu huku wawili kati yao hali zao zikiwa mbaya. Pia magari madogo manne yalipondeka baada ya kufukiwa na kifusi.

Tukio hili limetokea wakati serikali ikiwa bado haijachukua hatua za kurekebisha kasoro zilizobainishwa na tume iliyoundwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa baada ya kuporomoka kwa ghorofa la Chang’ome Village Hoteli Inn mwaka 2006 na kuua mtu mmoja.

Tume hiyo ilibaini kuwa zaidi ya maghorofa 100 jijini Dar es Salaam yalikuwa yamejengwa kinyume na taratibu za ujenzi. Kati ya maghorofa 505 ambayo waliyakagua, 147 yalikutwa hayana nyaraka za ujenzi.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliliambia Bunge kuwa tume hiyo ya Lowassa ilibaini kuwa katika ukaguzi huo pia maghorofa 81 yalikutwa yamekiuka masharti ya ujenzi huku mengine 22 wenyewe hawakupatikana na yalikuwa yamejengwa bila kuzingatia sheria za ujenzi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top