Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli,Mh. Edward
Lowassa akiweka shada la maua kaburini.
Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli,Mh.
Edward Lowassa akiongoza viongozi wenzake kwenda kwenda kuweka udongo
kaburini.nyuma yake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mh.
Bernard Membe.
Mwenyekiti wa makampuni ya IPP,Dr. Reginald
Mengi naye akiweka udongo kaburini.
*********
Waziri Mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli,Mh.
Edward Lowassa ameongoza maelfu ya Wakazi wa mji wa Arusha na mikoa ya jirani
katika mazishi ya mfanyabiashara na Kada maarufu wa CCM Mkoani Arusha,Marehemu
Henry Nyiti,nyumbani kwake Tengeru Arusha .
Nyiti alifariki ghafla wiki iliyopita akiwa
katika mgodi wake wa madini,Mahenge Mkoani Morogoro.
Wengine walioudhuria katika mazishi hayo ni
pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mh. Bernard
Membe,Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mh. Lazaro Nyalandu,Mwenyekiti wa
Makampuni ya IPP,Dr. Reginald Mengi,Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mh. Magesa
Mulongo,Mwenyekiti wa Chadema,Mh. Freeman Mbowe na Ridhiwani Kikwete.
credits: Othman Michuzi
Post a Comment