Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZAZI WAITAKA SERIKALI KUMUONDOA MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI SARANGA HARAKA

WAZAZI wa Kata ya Saranga wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam wameitaka serikali kumuondoa haraka Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Saranga kwa madai kuwa hana sifa za uwalimu, vyeti vyake vinaonesha kuwa ana taaluma ya uuguzi.
 
Akizungumza na wandishi wa habari jijini jana, Diwani wa Kata hiyo, Efraim Kinyafu (Chadema), alisema wazazi hao pia walikuwa wakishangazwa na shule hiyo kuendeshwa bila ya kuwa na Kamati kwa kipindi cha miaka minne huku mwalimu huyo akikwepa kukutana na viongozi mbalimbali walipotaka kukutana naye.
 
Alisema uamuzi huo, ulitokana na matokeo mabaya kitaaluma katika shule hiyo, hali iliyowafanya wazazi hao kuchunguza uwezo wa mwalimu huyo na kubaini kuwa hakuwa na sifa ya uwalimu bali aliingia kiujanja ujanja wakati shule hiyo inaanzishwa.
 
Kinyafu alisema wazazi hao waliuchukulia ukosefu wa taaluma kwa mwalimu huyo kuwa ni kikwazo cha maendeleo kitaaluma katika shule hiyo.
 
Hivyo wazazi hao waliadhimia kwa pamoja katika mkutano wao wa hadhara kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, kumuondoa mwalimu huyo na ikiwezekana amrudishe kwenye kazi yake ya kuhudumia wagonjwa hospitalini.
 
 “Kero nyingine zilizotajwa na wazazi hao ni kulazimisha michango bila kufuata taratibu za shule kujichukulia uamuzi wa kuwarudisha nyumbani watoto wanaoshindwa kulipia tuition na kushindwa kuwaheshimu viongozi wake katika wilaya hiyo”alisema Kinyafu. 
 
Alisema malalamiko kuhusu mwalimu huyo yanafahamika kutokana na mawasiliano ya mara kwa mara kati ya wazazi hao na mkurugenzi kupitia kwa diwani huyo.
 
Wakazi wa eneo hilo walikuwa na mkutano wa hadhara uliyofanyika kwenye viwanja vya shule hiyo ambapo mwalimu huyo pamoja na kupewa jukumu la kuwasambaza taarifa kwa wazazi, alishindwa kuhudhuria bila ya taarifa yoyote.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top