Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI OLE MEDEYE ATOA ANGALIZO


372 NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA
 Naibu waziri wa nyumba,ardhi na makazi ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Arumeru Magharibi,Goodlucky Ole Medeye amezitaka Serikali za Mitaa ukiwemo Uongozi wa Vijiji Mbalimbali ndani ya jimbo hilo kuhakikisha kuwa kamwe hawaangilii shuguli au miradi mbalimbali ya Wafadhili ambayo ina malengo ya kuwasaidia wananchi
 Medeye aliyasema hayo Jimboni humo wakati akizundua zahanati  ya Ester iliopo katika Kijiji cha Ngaramtoni ambayo ilijengwa kwa nguvu za wafadhili kutoka nchini Uingereza kwa malengo ya kudumisha sekta ya afya hasa afya ya mama na mtoto
 Medeye alisema kuwa kuwa endapo kama Vijiji vitakuwa vinaingilia masuala ya Miradi ambayo imetolewa na wafadhili kwa malengo mbalimbali ni wazi kuwa malengo hayo yatakwama na badala yake umaskini ndio utakaokirhiri huku jamii ikibaki na mateso mengi
 Aliongeza kuwa kazi ya Serikali ya Kijiji ni kuhakikisha kuwa miradi hiyo inafanya kazi kwenye viwango vya hali ya juu kama yalivyokuwa malengo ya wafadhili  hivyo kama Serikali za kijiji zitafanya hivyo basi zitachangia sana mabadiliko tena ya hali ya juu huku mabadiliko hayo yakichangia kupungua kwa umaskini
 Akiongelea Mradi huo wa zahanati ambao utaweza kuwanufaisha wananchi zaidi ya elfu kumi alisema kuwa mbali na kuwanufaisha wananchi wa Kijiji hicho cha Ngaramtoni lakini pia utaweza kuwanufaisha wananchi wa jimbo hilo kwa ujumla hivyo baadhi ya wanasisasa wasitumie nafasi hiyo kwa kuwadanganya watu kuwa kuna ubaguzi baina ya watu na watu
 Awali wanawake ambao ndio walengwa wakubwa sana wa mradi huo walisema kuwa zahanati hiyo itaweza kuwasaidia kwa kuokoa afya zao kwani walikuwa wanalazimika kutembea Umbali wa zaidi ya Kilomita Kumi kwa ajili ya kutafuta huduma za afya hali ambayo wakati mwingine husababisha vifo
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top