Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WATANZANIA 342 WANUFAIKA NA UFADHILI WA MASOMO NJE YA NCHI KWA KUANZIA 2010

1

Jumla ya Watanzania 342 wamepata fursa ya kusoma masomo mbalimbali nje ya Tanzania kati ya mwaka 2010 hadi 2012.
Kauli hiyi imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Philipo Augustino Mulugo (Pichani) wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Gando, Mhe. Khalifa Suleiman Khalifa aliyetaka kujua ni vijana wangapi wamepata nafasi za masomo nje ya nchi kuanzia mwaka 2010-2012 na ni vijana wangapi kutoka Zanzibar pamoja na nchi gani walikwenda kusoma.
Mhe. Mulugo amesema kuwa katika kuwapatia ufadhili unaotolewa na vijana wanashindanishwa kwa kutumia vigezo vya kitaaluma, umri na uraia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, ameongeza kuwa kinachozingatiwa zaidi ni kigezo cha kitaaluma, mwombaji yoyote anayetimiza kigezo hicho anayo haki ya kunufaika na ufadhili bila kujali anatokea sehemu gani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mhe.Mulugo amebainisha kuwa kutokana na mwingiliano wa wananchi wa pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakuwa vigumu kutofautisha sehemu ya Jamhuri alipotokea muombaji.
“Napenda kusisitiza kuwa nafasi za masomo zinatolewa kwa ajili ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwamba wote wanashindanishwa kwa vigezo vya kitaaluma na si vinginevyo.
Katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2012, nchi ambazo zimekuwa zikitoa nafasi za masomo kwa Watanzania nje ya nchi ni Cuba, Algeria, Urusi, Msumbiji,Serbia, Uingereza, Misri, Korea Kusini, Macedonia, Uturuki, China, Ujerumani na Oman
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top