![]()  | 
| RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE | 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete 
leo, Jumatatu, Mei 6, 2013, ameamua kukatiza ziara yake ya Kiserikali 
nchini Kuwait ili kurejea nyumbani kutokana na tukio la shambulio la 
kigaidi la mlipuko mjini Arusha ambako watu wawili wamefariki na 60 
wamejeruhiwa.
Rais
 Kikwete aliyekuwa aondoke kesho kurejea nyumbani, amelazimika kukatiza 
ziara hiyo na anaondoka Kuwait City kurejea nyumbani mara moja ili kuwa 
karibu na wafiwa pamoja na wale waliojeruhiwa katika shambulio hilo la 
kigaidi.
Miongoni
 mwa shughuli ambazo hazitafanyika sasa kutokana na uamuzi huo wa Rais 
ni ziara ya kutembelea Kampuni ya Mafuta ya Kuwait katika  eneo la 
Ahmadi mjini Kuwait. Aidha, Rais hatahudhuria dhifa ya chakula cha jioni
 ambacho alikuwa anaandaliwa na Waziri Mkuu wa Kuwait, Mheshimiwa Sheikh
 Jaber Al Mubarak Al Hamad Al Sabah.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6 Mei, 2013



Post a Comment