Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Majambazi watano walioiba fedha wakamatwa


JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwakamata majambazi watano waliopora Sh 46,000,000 maeneo ya Mbagala Rangi Tatu. Akizungumza Dar es Salaam jana, Kamanda wa Kanda hiyo, Suleimani Kova, alisema mfanyabiashara mmoja akiwa katika duka lake la kuuza bia za jumla akiwa na fedha hizo alizoweka ndani ya boksi kwa ajili ya kuzipeleka Benki ya BOA ghafla alivamiwa na majambazi wanne huku watatu wakiwa na bunduki kubwa moja na bastola mbili wakiwa wametumia pikipiki mbili aina ya Boxer na baaada ya polisi kupata taarifa hizo waliwafuatilia majambazi hao na kufanikiwa kuwakamata maeneo ya Chamanzi.
Alitaja majina ya watuhumiwa wote waliohusika na tukio hilo kuwa ni Bernad Yohana, Steven Thadeo, Adam Isidory, Jonh Benja na Sultan Kipensa wote wakiwa wamekiri kuhusika na uporaji huo na kumtaja mwenzao John Tesha kuwa ndiye aliyekimbia na fedha hizo.


Katika tukio jingine, wanamshikiria Eric Mbisa kwa kukutwa na pikipiki moja aina ya Fekon yenye rangi nyeusi na ina namba za usajili T 155 CHX pamoja na pingu na ametambuliwa kuhusika na matukio mbalimbali ya wizi wa pikipiki.

Alisema kuna baadhi ya pikipiki zinatumika katika uhalifu hasa aina ya Boxer kwa kuwa zina uwezo mkubwa wa kukimbia hivyo pikipiki zote za aina hiyo zitafuatiliwa na kuchukuliwa hatua zile zote zinazotumika bila ya vielelezo.

Alisema kuna baadhi ya pikipiki 300 tayari zimekamatwa na kati ya hizo 201 ni aina ya Boxer hivyo pikipiki zote aina hiyo zinatiliwa shaka kwa kuwa zinatumika katika ujambazi.

Alisema pikipiki zote zitawekwa alama kama teksi kwa ajili kugundulika na zitakapotumika kwa uhalifu iwe rahisi kujulikana.


MTANZANIA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top