Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MANUMBA AREJEA KAZINI RASMI

 


Hatimaye hali ya afya ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Nchini, Robert Manumba(Pichani juu), imeimarika na amerejea kazini, limeandika Mwananchi Akizungumza kwa njia ya simu, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso, alikiri kuwa Manumba amereje kazi ingawa hakuwa tayari kutaja tarehe aliyoingia kazini.“ Eh! Unauliza nini, mbona ameanza kazi siku nyingi, siwezi kukumbuka tarehe sipo ofisini naelekea kwenye kikao cha kazi,” alisema Senso.Habari za kuaminika kutoka kwa baadhi ya maofisa wa kitengo cha upelelezi, zilisema kiongozi huyo ameshaanza kazi baada ya afya yake kutengemaa.Manumba mwenyewe, kifupi alisema “Kwa sasa sijambo, ninakwenda kwenye mkutano.” Mkurugenzi huyo alirejea nchini April 22, mwaka huu akitokea Afrika Kusini alikokuwa akitibiwa katika Hospitali ya Millpark.
Amekuwa katika hospitali hiyo kwa zaidi ya miezi miwili, kuanzia Januari 26, mwaka huu akisumbuliwa na malaria.
Hatua ya kumpeleka Afrika Kusini, ilikuja baada ya kulazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi katika Hospitali ya Aga Khan Januari 13, mwaka huu, akiwa hajitambui,.Alikuwa akipumua kwa msaada wa mashine.
na viongozi mbalimbali wakiwamo wa Serikali walikwenda kumjulia hali.
Manumba amerejea baada ya madaktari waliokuwa wakimtibu kujiridhisha juu ya kuimarika kwa afya yake.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top