Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MARTHA GEWE ANYAKUA TAJI LA REDD'S MISS UKONGA 2013

 


Mshindi wa Shindano la Redd’s Miss Ukonga 2013, Martha Gewe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili, Diana Joachim (kushoto) pamoja na mrembo aliyeshika nafasi ya tatu, Natasha Mohamed mara baada ya warembo hao kutangazwa kuwa ndio washindi wa shindano hilo Usiku wa kuamkia jana katika shindano lililofanyika Ukumbi wa Wenge Garden Ukonga Mombasa jijini Dar es Salaam. Martha aliwashinda warembo wengine 12 katika shindano hilo.
Warembo waliofanikiwa kuingia hatua ya tano bora ya Redd’s Miss Ukonga 2013 wakiwa katika picha ya pamoja kutoka kushoto ni Vanesa Magile, Matha Gewe, Diana Joachim, Natasha Mohamed na Nancy Abasy shindano lilifanyika Ukumbi wa Wenge Garden Ukonga Mombasa jijini Dar es Salaam. Martha.
Baadhi ya washiriki wa Shindano la Redd’s Miss Ukonga 2013 wakicheza show ya ufunguzi wa shindano lao lililofanyika usiku wa kuamkia jana katika ukumbi wa Wenge Garden Ukonga jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya majaji wa shindano hilo wakiongozwa na William Malecela 'Le Mutuz' (mwenye kofia) wakifuatilia shindano hilo kwa umakini.
Gwiji wa Mipasho nchini Tanzania, Malkia Hadija Omar Kopa aliongoza upande wa Burudani na kukonga nyoyo za mashabiki wake na wa sanaa ya urembo katika eneo la Ukonga na viunga vyake.
Baadhi ya warembo wa Ukonga walioshiriki shindano hilo 2012 na katikati ndiye aliyevua taji jana Elizabeth.
Warembo mbalimbal;i walioshiriki Redd's Miss Ukonga wakijinadi na vazi la ubunifu jukwaani.
Martha Gewe akijinadi na kivazi cha Ufukweni
Annatolia Raphael nae alirusha kete yake jukwaani na vazi la ufukweni.
B Band ikiongozwa na Mtanashati, Banana Zahiri Ali Zoro nayo ilikuwepo ndani ya Wenge Garden Ukonga Mombasa kusindikiza vilivyo show hiyo.
Redd's Miss Tanzania aliyeshika nafasi ya pili 2012, Eugenia (kushoto) nawashiriki wenzake wa shindano hilo mwaka jana walikuwepo Ukonga.
Redd's Miss Tabata 2013 nao walifika kujitambulisha na kuwakaribisha wana Ukonga katika onesho lao litakalofanyika Ijumaa katika ukumbu wa DarWest Park Tabata. Warembo hawa muda huu wapo Mikumi kwa ziara ya kutalii.
Baada ya kupita jukwaani na vazi la usiku washiriki wote wa Redd's Miss Ukonga 2013 walijipanga jukwaani.
Mgeni rasmi Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa (katikati), Mdau wa Miss Ukonga Daud Mambya (kushoto) pamoja na Regina Ogwal wakifuatilia matukio katika shindano hilo.
Jaji Mkuu wa Shindano hilo William Malecela akitangaza majina ya washindi.
Mgeni rasmi Diwani wa Kata ya Kipawa, Bonnah Kaluwa (katikati), Mdau wa Miss Ukonga Daud Mambya (kushoto) pamoja na mmoja wa wadhamini wa Shindano hilo, Kampuni ya Mambya Insurance, John Mambya wakifuatilia shindano.
Ofisa Habari wa Kamati ya Miss Tanzania, Hidan Ricco (kulia) akiwa pamoja na Mwandaaji wa Miss Tabata, Fredy Ogot na Mwandaaji wa Miss Moshi, Jacqueline Chuwa.
 
CREDITS: FATHER KIDEVU
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top