Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Matukio katika picha kwenye mkutano wa wizara ya mambo ya ndani na idara zake mjini Morogoro leo

 

    
Aliyekaa wa kwanza kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Jamii Bw. Fidelisi Mboya akifafanua jambo mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi   Mbarak Abdulwakil kuhusu zoezi la Uandaaji wa Mpango kazi na Ununuzi kwa ajili ya Idara yake kama sehemu ya maandalizi ya Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2013/2014 aliyekaa katikati ni Afisa Bajeti wa Idara ya Sera na Mipango  wa Wizara hiyo Michael Msikila  pembeni yake ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Huduma kwa Jamii Bw. Aloyce Msika.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.
_DSC0258
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil akikagua zoezi la Uandaaji wa  Mpango kazi na Ununuzi wa  Idara ya Magereza akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Bajeti wa Idara ya Magereza ikiwa ni maandalizi ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2013/2014.

_DSC0270
Sehemu ya Maafisa Bajeti wa Idara ya Zimamoto na Uokoaji wakipokea maelekezo muhimu  kutoka kwa  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil aliyesimama,  baada ya Katibu Mkuu huyo kukagua Mpango kazi na Ununuzi wa Idara hiyo katika kikao kazi kinachoendelea mjini Morogoro.
_DSC0305
Baadhi ya Maafisa Bajeti wa Jeshi la Polisi wakipokea maelekezo muhimu kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo  ya Ndani  ya Nchi Mbarak Abdulwakil aliyesimama baada ya Katibu Mkuu huyo kukagua Mpango kazi na Ununuzi unaoandaliwa na Maafisa hao wa Bajeti ikiwa ni sehemu ya Maandalizi ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2013/2014.
 _DSC0319
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi aliyesimama akitoa Maelekezo kwa Maafisa Bajeti wa Idara ya Utawala na Rasilimali  Watu  baada ya kukagua Mpango kazi na Ununuzi wa Idara hiyo unaondaliwa na Maafisa bajeti hao, katika kikao cha kuandaa Mpango kazi na Ununuzi kinachotarajiwa kumalizika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro. _DSC0332
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil  aliyesimama akikagua kazi ya Maandalizi ya Mpango Kazi wa Idara ya Uhamiaji  katika kikao cha kuandaa mpango kazi huo kinachoendelea mjini Morogoro, anayemtazama ni Kamishna  wa Utawala na Fedha wa Idara ya Uhamiaji Piniel Mgonja   wa pili kutoka kushoto ni Mhasibu Mkuu wa Idara ya Uhamiaji P. Kabale.kikao hicho ni sehemu ya utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa fedha 2013/2014. 0227
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil  watatu kutoka kulia waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wakuu wa wizara  hiyo, Makamishna, Maafisa Bajeti na Ugavi na Ununuzi wa wizara hiyo wanaohudhuria kikao kazi cha kuandaa Mpango Kazi na Ununuzi wa wizara hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa fedha 2013/2014, wa pili kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mwamini Malemi na wa pili kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu Lilian Mapfa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top