
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Kamishna Jenerali Evaristus Shikongo akiijaribu moja ya silaha inayotumika kwa ajili ya kutuliza ghasia wakati wowote inapotokea ndani na nje ya gereza

Askari wa Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani, wakimuonesha mbinu za kupambana na adui pasipo kutumia silaha Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia,

Mkuu wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, ACP Mbaraka Semwanza akitoa taarifa fupi ya chuo hicho kwa Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Kamishna Jenerali Evaristus Shikongo (katikati). Kushoto aliyekaa ni Kamishna wa Sheria na Utawala wa Jeshi la Magereza, Dk Juma Malewa, kulia ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga, anayefuata ni Kamishna wa Rasilimali Watu, Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Clementine Feris. Picha na Felix Mwagara.

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja (kushoto) na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Kamishna Jenerali Evaristus Shikongo wakionyesha taarifa ya makubaliano waliyosaini.
Post a Comment