Na Hassan Silayo – MAELEZO
SHIRIKA
la Vijana wa Afrika (YOA) lenye makao yake jijini Dar es Salaam,
linaandaa tuzo kwa ajili ya vijana walio chini ya umri wa miaka 30
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo Bwana Awadh Milasi
wakati akiongea na waandishi wahabari leo(jana) jijini Dar es Salaam.
Awadh alisema kuwa tuzo hizo zitatokana vipaumbele nane ambavyo ni Habari,Ujasiriamali,Uvumbuzi,
Mitindo ya mavazi,Michezo,Sanaa na Ubunifu,Burudani na Mchango kwa jamii ambayo ndiyo tuzo kuu.
Alisema
kuwa lengo kuandaa tuzo hizo ni kuleta fikra chanya kwa vijana wengi
wa kitanzania ili kuibua vipaji na kupambana na changamoto hili
kuletea maendeleo.
Aidha aliongeza kuwa mchakato wa mapendekezo ya majina ya washiriki uko wazi kwa vijana wenye umri kati ya miaka 16 na 30
“Shilikaa
linapenda kufahamisha umma na vyombo vya habari kuwa mapendekezo sasa
yapo wazi kwa vijana wa kitanzania wenye umri kati ya miaka 16 na 30 kwa
kuzingatia vigezo vilivyoainishwa” Alisema Awadh.
Kwa
upande wake Afisa Rasilimali Fedha,Mushumba Avitus ameeleza nia yao ni
kushawishi na kutoa mchango kwa Serikali na mashirika yasiyo ya
kiserikali katika kutambua uwepo wa shughuli muhimu zinazofanywa na
vijana katika jamii
Mshumba
amesema vijana wenye uthubutu ni wakati wao wa kujitokeza na kushiriki
katika tuzo hizi ambapo alisema kuwa washiriki watapendekezwa kupitia
tovuti ya www.youthawards.or.tz ulionza tarehe 2 Mei hadi tarehe 7 Juni 2013.



Post a Comment