Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Anjela Kairuki azindua Ilani ya Katiba ya Wanawake TGNP

 

      
DSC_0544
Naibu Waziri wa Katiba na sheria, Mhe. Anjela Kairuki, amezindua rasmi,  Ilani ya Madai ya wanawake kwenye Katiba mpya leo katika viwanja vya mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP).
********
 Naibu waziri amewataka wanwake kukataa kutumika na wanasiasa kama daraja la kuwapistisha wao kushika madaraka. “ninawataka wanawake tukatae kutumika, hata sisi tunaweza, tumetumiwa sana kupitisha mambo ya watu wengine, waoa wananufaika sisi tuabaiki kulalamika,  umefika wakati na sisi tutumie fursa zilizopo kuhakikisha tunanufaika nazo na kupata naafsi ya ushiriki wa kutosha kwenye uongozi” amesema Kairuki
Ameongeza kuwa  wanwake wajitahidi kujitokeza katika kugombea nafasi za uongozi katika ngazi mbalimbali za uongozi na kuytumia mchakato wa Katiba mpya kama fursa ya kupata nafasi za kutosha kwenye uongozi, “Tusipoutumia huu mchakato kupata nafasi, tutajuta, kwa kipindi kirefu kumekuwepo na malalamiko kuwa hatupewi nafasi, lakini huu mchakato wa Katiba unapita lazima tuutumie kufanikisha ajenda zetu wanawake na kuunganisha nguvu za pamopja katika kudai mgawanyo sawa wwa rasilimali za taifa hil”
 Mhe. Kairuki amewataka wanawake kuhakikisha wanaungana na kutokukubali kugawanywa au kujigawa kimakundi.
Amesema kuwa kila mwanamke ajitahidi kuisoma ilani ya madai iliyoandaliwa na TGNP ili kubeba agenda za wanawake kwenye mijadala inayoendela ya kujadili rasimu ya katiba kwenye mabaraza ya katiba mara yatakapoanza.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Ussu Mallya alisema TGNP kwa kushirikiana na wanaharakati wa masuala ya ukombozi wa wanawake, usawa wa kijinsia, haki za Binadamu, utawala bora na Maendeleo wamekuwa na utaratibu wa kuandaa ilani mbalimbali za wananchi kuanzia uchaguzi wa mwaka 2000, 2005 na 2010.
 “Mwaka huu tumeandaa Ilani ya madai ya wanawake wa Tanzania kwenye katiba mpya, ili kuwezesha jamii kuchambua, kujadili na kuangalia maeneo muhimu ya kudai uwajibikaji na utekelezaji wakati wa mijadala ya kuandaa katiba mpya.
Alisema mchakato wa kuandaa madai ya katiba mpya umetokana na ushiriki mkubwa wa wadau mbalimbali yakiwemo mashirika katika ngazi ya kitaifa na jamii yanayotetea haki za Binadamu, jinsia na maendeleo, Femact na GDSS ambazo hufanyika kila Jumatano mabibo.
Kwa mujibu wa Mallya alisema madai hayo yametokana na ushiriki na sauti mbalimbali za wadau wanaotetea haki za wanawake na hususani haki zao za kikatiba na kuongeza kuwa ni matumaini yao kuwa tume ya mabadiliko ya katiba inatambua changamoto zinazowakabili wanawake ili yaweze kuingizwa katika katiba mpya.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top