Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RUNGWE WAJADILI KUHUSU KUUGAWA MKOA WA MBEYA

 







MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA RUNGWE AKIONGEA NA BARAZA LA MADIWANI NA WATENDAJI KATIKA KIKAO MAALUM CHA KUUUGAWA MKOA WA MBEYA KUWA MIKOA MIWILI
MWENYEKITI WA KIKAO MAALUM CHA BARAZA LA MADIWANI RUNGWE ALFRED MWAKIPIKI AKATOA TAMKO KUWA MAKAO MAKUU YA MKOA MPYA UWE TUKUYU, NA MAPENDEKEZO YA WILAYA YAKIWA NI 1. RUNGWE 2. ILEJE 3. KYELA 4. BUSOKELO ITAMBULIKE KAMA WILAYA ILI KUUNDA MKOA WENYE WILAYA NNE
DAS ALINANUSWE MWALUFUNDA AKITOA TAARIFA YA SERIKALI BAADA YA MCHAKATO HUU KUANZA ILI KUGAWA MKOA WA MBEYA NA KUWA MIKOA MIWILI
Afisa utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ndugu Mbai akisoma mapendekezo ya wilaya ya Rungwe kwa madiwani wa Halmashauri ya wilya ya Rungwe kwa ajili ya kuugawa mkoa wa Mbeya.

Mmoja wa madiwani ndani ya baraza hilo ndugu Anyimile Mwasakilali Kata ya Kawetere( NCCR) kupinga vikali suala la ugwaji wa mkoa mbeya kutokana na kuwepo kwa changamoto mbalimbali zinazo ikabili wilaya hiyo ya Rungwe
Diwani wa kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe. Bashiru Madodi akichangia hoja ya kuugawa mkoa wa Mbeya
JENGO LA OFISI YA HALMASAHURI YA RUNGWE



Kitendo cha serikali kusogeza madaraka kwa karibu zaidi na wananchi ili kuwawezesha kuamua mambo yanayo husu maisha maendeleo ya kila siku imechangia kwa asilimia kubwa baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Runwe kuamua kutumia hoja hiyo kuugawa mkoa mbeya na kuwa mikoa miwili.

Moja ya sababu ambazo zimepelekea baraza hilo kutumia hoja hiyo kama kigezo mojawapo cha kujipatia mkoa mpya ni pamoja na kupanga kubuni na kutekeleza kulinda na kuendesha mipango yao kwa kutekelezwa kitaalamu zaidi katika kuwaletea maendeleo wananchi endapo mkoa huo utapatikana.

Hatua hiyo imefikiwa katika kikao maalumu cha baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kilicho keti kujadili mpango wa ugawaji wa Mkoa wa mbeya kuwa mikoa miwili ambapo katika katika kikao hicho baraza hilo la madiwani limefikia maamuzi ya kuugawa mkoa huo wa mbeya na kuuita mkoa wa Rungwe ambapo makao makuu yake yamependekezwa kuwa Mamlaka ya mji mdogo Tukuyu.

Akiwasilisha mapendekezo ya kamati tendaji( CMT) na kamati ya fedha Ndugu Noel Mahyenga amesema wanaipongeza serikali ya awamu hii kwa hatua yake ya kukubali kutoa mapendekezo yake ya ugwaji wa mkoa wa mbeya kwa lengo la kupunguza mzigo na majukumu Ya serikali kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi.

Amesema katika kufanya hayo serikali imekuwa ikigawa mikoa wilaya na Halmashauri ili kurahisisha utawala na uendeshaji wa taasisi hizo katika hatua moja wapo ya utekelezaji wa malengo yake yaliyokusudiwa.

Wamesema kulingana na ukubwa wa eneo na idadi ya watu katika mkoa huo wa mbeya imekuwa vigumu kwa watumishiwaliopo sekretalieti ya mkoa kusimamia kikamilifu maendeleo ya mkoa kwa maana ya kutoa ushauri wa kitaalamu pamoja na kusimamia utekelezaji wa shughuli mablimbali za kimaendeleo kwa wakati muafaka ili kukidhi haja inayokuwepo wakati inapo hitajika.

Hata hivyo baraza hilo kwa nguvu moja limekubali kutoa moja ya majengo yake mapya yaliyojengwa ndani ya halimashauri hiyo kuwa ofisi ya mkoa ambapo ujenzi huo umetumia fedha za ndani pamoja na baraza hilo pia limependekeza halmashauri ya wilaya ya busokelo iwe wilaya ili kufanya mkoa kuwa na wilaya nne ambazo ni Kyela,Ileje na Busokelo badala ya wilya tatu zilizopo hivi sasa.

Pamoja na baraza zima la halmashauri hiyo kupitisha hoja hiyo ya ugawaji wa mkoa mmoja wa madiwani ndani ya baraza hilo ndugu Anyimile Mwasakilali Kata ya Kawetere( NCCR) kupinga vikali suala la ugwaji wa mkoa mbeya kutokana na kuwepo kwa changamoto mbalimbali zinazo ikabili wilaya hiyo.

Moja ya changamoto hizo ni pamoja na kata yake kuto patiwa ofisi ya Afisa Mtendaji kwa muda mrefu sasa hivyo amehoji juu ya kuanzishwa kwa mkoa mpaya wakati bado kuna changamoto nyingi hivyo kitendo cha hatua hiyo kitawabebesha mzigo mkubwa wananchi wake pamoja na serikali kwa ujumla.
Mbeya yetu
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top