RAIS 
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete anatarajia kuzindua 
ujenzi wa barabara na kufungua rasmi kivuko cha Ruvuvu mkoani Kagera.
Taarifa
 ilio tolewa na Katibu mkuu wa wizara ya Ujenzi Balozi Herbert Mrango 
kwa yvombo vya habari inasema kuwa Mheshimiwa Raisi Kikwete atazindua 
kivuko hicho Julai 27 mwaka huu.
Kivuko
 hicho chenye uwezo wa kubeba tani 35 ikiwemo magari madogo 4 na abiria 
80 kwa pamoja,  kinatoa huduma ya kuvusha magari na abiria katika mto 
Ruvuvu eneo la Rusumo
Alisema
 kabla ya ufunguzi wa kivuko hicho, Rais Kikwete ataweka jiwe la msingi 
kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Kigoma-Biharamulo-Lusahunga yenye 
urfu wa kilometa 154, Julai 26 mwaka huu.
“Jumapili
 tarehe 28 Julai Rais Kikwete ataweka jiwe la msingi katika barabara ya 
Kyaka-Bugene-Kasumulo yenye urefu wa kilometa 59.1 tukio litakalofanyika
 katika kijiji cha Omugakorongo” alisema Balozi Mrango.
Alifafanua
 miradi yote mitatu inagharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa 
Tanzania na kwamba kutekelezwa kwa miradi hiyo itasaidia sekta ya 
usafirishaji na kukuza uchumi wa mkoa wa Kagera.
Aliongeza
 kuwa barabara na kivuko hicho vitaimarisha huduma ya usafirishaji 
katika mkoa huo na kuboresha biashara na usafiri kati ya mkoa huo na 
mikoa mingine pamoja na nchi za Burundi, Rwanda na Uganda

 


.jpeg) 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment