Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Muungano wa Wanajeshi wastaafu Tanzania”MUWAWATA” watoa ya moyoni

 

  
SONY DSC
 
Mwenyekiti wa Muungano wa Wanajeshi wastaafu Tanzania (MUWAWATA),Assedy Rajabu  Mayungi(kilia)akitoa tamko mbele ya waandhi wa habari (hawapo pichani) jana kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo jijini Dar es salaam,kuzuia mikutano isiyo halali ya watu wanaopotosha MUWAWATA(katikati)Mjumbe,Lenson Tupate(kulia)Mjumbe.Chalesi Sabugo.
Na Philemoni Solomon wa fullshangwe
“Ninatamka kwamba kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi mkuu wa MUWAWATA TAIFA uliofanyika tarehe 20/10/2013 mjini Dodoma ambao ndio ulioniweka madarakani bado ninaendelea kuwa Mwenyekiti wa MUWAWATA TAIFA mpaka pale kipindi changu cha miaka mitano kukaa madarakani kitakapomaliziaka kwa mujibu wa sheria na si vingenevyo,na hii inatokana na katiba ya MUWAWATA kwa mujibu wa cheti cha usajili Namba S.A.17184 ACT.CAP 337 C.R.E.2002 kilichotolewa tarehe 27/12/2012 na msajili wa vyama hiari toka Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi”alisema Mayungi,
Aliendelea kusema,kuanzia tarehe ya leo mikutano yote ya Taifa,Mikoa,Wilaya na kata inayofanywa na kikundi haramu kinachojiita kamati ya MUWAWATA mapito ambayo haipo kikatiba isifanyike,wanachama wa MUWAWATA mnapotoshwa na kundi hilo,kikao chochote kitakachofanyika baada ya tamko hili ni batili na hatua kali za kisheria zitachukuliwa mara moja,fomu zilizoandaliwa na kikundi hicho pamoja na kadi ni batili msikubali kwa sababu siyo nyaraka halali za MUWAWATA vile vile nyaraka zilizosambazwa kupitia mitandao yao ya kijamii pia ni batili,taarifa zilizosambazwa za kufanyika Mkutano uwanja wa ndani wa Taifa tarehe 3,Augost,2013 siyo za MUWAWATA na mkutano huo siyo halali,uongozi wa MUWAWATA bado unawasiliana na serikali ili kuweza kupata majibu ya malalamiko ya ufinyu wa pensheni ya Wastaafu kwani bado serikali inatujali juu ya suala hilo”,alisema Mayungi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top