Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KATIBU MKUU WA CCM ABULRAHMAN KINANA AENDELEA NA ZIARA YAKE SHINYANGA VIJIJINI LEO

01

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye wakishiriki katika ujenzi wa Birika la Kunyweshea mifugo linalojengwa katika Kata ya Didia Jimbo la Solwa Katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga vijijini mkoani Shinyanga, ambapo leo katibu Mkuu huyo ameendelea na ziara yake ya siku nne mkoani humo na kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo katika kuimarisha uhai wa chama hicho na utekelezaji wa Ilani ya ya Uchaguzi.PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE -SHINYANGA. 1
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Mbunge wa jimbo la Solwa Ahmed Salum wakicheza na nyoka pamoja na wanakukundi cha utamaduni kutoka jimboni humo.
 2
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja akimlipa ujira wa shilingi elfu 10.000 Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye baada ya kumsaidia katika ujenzi wa Birika la kunweshea mifugo katika kata ya Didia, hata hivyo Kinana aliwapa fedha pia wajenzi wa birika hilo. 4
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wakati alipokagua ujenzi wa Soko la Kata ya Didia lililojengwa katika kijiji cha Didia, kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga Ndugu Khamis Mngeja.
 5
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana akipiga picha ya pamoja na viongozi mbalimbali mbele ya soko hilo. 8
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Vijijini Bw.Kiyungi Mohamde Kiyungi wakati alipokagua ujeni wa Hospitali ya Halmashauri hiyo inayojengwa katika kijiji cha Iselamagazi, wa tatu kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga Ndugu Khamis Mngeja. 12
Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akicheza na nyoka wakati aliposhiriki katika kucheza ngoma ya asili katika kijiji cha Didia. 14
Hili ndilo soko la Didia 16
Wapiga ngoma wa Kikundi cha ngoma cha Didia wakipiga ngoma wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokagua ujenzi wa soko la Didia. 18
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi waliomsimamisha katika kijiji cha Mwabenda ambao walikuwa na mabango yaliyokuwa yakielezea kero zao katika kijiji hicho ambazo zilikuwa ni Umeme na maji hata hivyo mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ndugu Ally Rufunga aliwaelezea mipango ya serikali kuhusu kijiji hicho katika kuhakikisha maji na umeme vinapatikana mapema katika kijiji hicho. 19
Kikundi cha ngoma kikitumbuiza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Salawe katika jimbo la Solwa mkoani Shinyanga. 21
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtunza mmoja wa wasanii wa kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitumbiza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Salawe katika jimbo la Solwa mkoani Shinyanga. 22
Wananchi wakiwa wamehudhuria kwa wingi katika mkutano huo wa hadhara.
26
MNEC Azza Hilal Hamad kutoka Viti Maalum mkoa wa Shinyanga akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara kijijini Salawe. 27
Mbunge wa jimbo la Solwa Ahmed Salum akiwahutubia wapiga kura wake katika kijiji cha Salawe ambapo mkutano wa hadhara umefanyika leo. 28
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika kijiji cha Salawe ambapo mkutano wa hadhara umefanyika leo.

 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kwenye ujenzi wa Birika la kunyweshea mifugo katika kata ya Didia.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na mafundi ujenzi wanaoshiriki kujenga birika la kunyweshea maji mifugo katika kata ya Didia.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa akitoa ushirikiano wa kutosha kutoka kwa mwananchi aliyeomba kupiga nae picha nje ya soko jipya katika kata ya Didia.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi baada ya kutembelea soko la jipya katika kata ya Didia na kuwapongeza sana wakazi wa kata hiyo kwa kushirikiana na uongozi wake kwa kufanikisha ujenzi wa soko hilo.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa amebeba nyoka aina ya chatu nje ya jengo la soko jipya katika kata ya Didia, Nyoka huyo huchezwa kwenye ngoma inayoitwa Wagoyangi.
 Katibu Mkuu akipata maelezo juu ya maendeleo ya ujenzi wa hospitali ktika kata ya Iselamagazi.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi wa kata ya Iselmagazi wakati wa ziara yake ya wilaya ya Shinyanga Vijijini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongea na Juma Mayenze mkazi wa kijiji cha Mwasekagi kata ya Solwa ambaye alikuwa anamfikishia ujumbe juu ya tatizo la maji na umeme kijijini hapo.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili uwanja wa mkutano katika kata ya Salawe.

 Wasanii wa kikundi cha Tangawizi wakionyesha sanaa yenye stori nzuri iliyoonekana kufunza uelewa wa hatua za maendeleo ya Mtanzania tangia wakati wa mkoloni mpaka sasa.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia umati wa wakati wa kata ya Salawe na maeneoya jirani waliofika kusikiliza sera na misimamo imara ya Chama Cha Mapinduzi.
 Mbunge wa Viti Maalum  Azah Hilal Hamad akihutubia wananchi  kwenye mkutano wa hadhara na kuelezea namna gani serikali sikivu ya CCM inavyojali wananchi wake.
 Mbunge wa Solwa ndugu Ahmed Salum akihutubia wananchi wake na kuelezea namna utekelezaji wa ilani ya uchaguzi unavyoenda vizuri .
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa wilaya ya Shinyanga Vijijini .

 Ngoma ya Kucheza na Fisi ilikuwa na kivutio cha aina yake  katika viwanja vya Salawe.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akikata papai huku Katibu wa NEC Itikadi na Unezi akichukua kipande kingine  cha papai ,Katibu Mkuu pamoja na Katibu wa Uenezi walikuwa kwenye ziara yao ya kujenga na kukiimarisha chama katika  wilaya ya Shinyanga Vijijini.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top