Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS WA NIGERIA AWATIMUA KAZI MAWAZIRI WAKE

                                                               

130515090435 goodluck jonathan 304x171 afp nocredit 1603aRais wa Nigeria Goodluck Jonathan amewafuta kazi mawaziri tisa katika hatua yake ya kwanza kubwa ya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri.
Ni mara ya kwanza tangu kuchaguliwa miaka miwili iliyopita, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa serikali hii leo. Hata hivyo taarifa hii inakuja wakati kuna migawanyiko mikubwa katika serikali
Mawaziri walioachishwa kazi ni pamoja na waziri wa mambo ya nje, elimu, waziri wa Sayansi na teknolojia , waziri wa makaazi na ustawi wa miji, waziri wa mipango ya serikali na mazingira
Mawaziri wengine waliofutwa kazi ni ule wa mambo ya ndani na manaibu waziri wa kawi na kilimo pamoja na ulinzi ambao pia waliachishwa kazi.
Taarifa zilisema kuwa mawaziri wapya watateuliwa lakini mara moja.

Wiki mbili zilizopita magavana saba wenye ushahwishi mkubwa sana pamoja na aliyekuwa makamu wa rais Atiku Abubakar waliunda vuguvugu lao pakee na kujitenga na chama tawala
Walighadhabishwa na hatua ya washirika wao kunyimwa fursa ya kugombea nyadhifa za kisiasa katika chama tawala.
Wadadisi wanasema kuwa ugomvi unatokana na wanasiasa kuanza kujipanga au kujiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015
Chama cha kitaifa kimeshinda uchaguzi wote wa kitaifa tangu mwaka 1999 mwishoni wa utawala wa kijeshi kwa hivyo kiongozi wa chama ambaye ni Godluck Jonathan atakuwa na fursa nzuri ya kushinda kwenye uchaguzi huo.
chanzo bbc.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top