Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kinana aagiza mikataba uchumi CCM ‘ianikwe’

Katibu Mkuu wa CCM, Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana, amezitaka ofisi za chama hicho wilayani na mikoani kuhakikisha mikataba yote ya uchumi ambayo wanaingia inakuwa wazi kwa wanachama.
             
Akizungmza baada ya kuwasili Nzega, mkoani Tabora jana, Kinana alisema hatua hiyo itaondoa mikataba hiyo kuwanufaisha watu wachache.

Kinana aliyasema hayo baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa mabanda 54 kuzunguka Uwanja wa Michezo wa Samora, unaomilikiwa na chama hicho Wilaya ya Nzega.

Ujenzi huo utakapokamilika mabanda hayo yatakodishwa kwa wafanyabiashara watakaolipa kodi CCM.

Alisema mikataba yote iwe wazi na taarifa zake ziwasilishwe kwenye vikao mahsus, ili wanaotaka kuhoji wafanye hivyo.


Katika hatua nyingine, Kinana alimmwagia sifa Mbunge wa Nzega, Dk Khamis Kigwangallah, akimtaja kuwa mchapaka kazi ambaye hachoki, huku wananchi waliohudhuria wakimtaja mbunge huyo kuwa ni ‘jembe.’

Awali, akisoma taarifa ya mradi huo, Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM Wilaya ya Nzega, Majaliwa Bilal, alisema mradi huo unatekelezwa kwa utaratibu wa wafanyabiashatra kujenga vibanda hivyo kwa gharama zao. MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top