Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KINGUNGE AWAFUNDA WANA MTWARA

Wakazi wa Mtwara wameshauriwa kujenga umoja na mshikamano ili kuona  jinsi wanavyoweza kufanya maendeleo yao.
             
Akizungumza kwenye semina ya viongozi wanawake Mkoa wa Mtwara juzi, Mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale-Mwiru, aliwasihi wakazi wa Mtwara kuwa na umoja na mshikamano, kuona jinsi watakavyofaidika na mradi wa gesi.

Hata hivyo, Kingunge hakutaka kuzungumzia zaidi masuala ya gesi kwa kile alichokidai hana elimu nayo, hivyo kutaka mjadala wa katiba uendelee bila kuingiliwa.

“Gesi siwezi kuizungumzia sana, ila ikitumika vizuri itasaidia kusukuma mbele maendeleo ya watu, hivyo kinachotakiwa ni sera ya uwezeshaji wananchi kuona jinsi  watu watakavyoshiriki kufaidika na gesi,” alisema.



Kingunge alisema hivi sasa watu wanajadili mambo ya Serikali tatu na vyeo, hawafikirii na kuzungumzia mambo ya msingi kama ufugaji, kuona jinsi wafugaji  watakavyosaidiwa.

 “Mjadala wa katiba uendelee, kwani walikofikia watu sasa wanajadili vyeo na Serikali tatu hakuna mustakabali wa watu kufikiria,” alisema Kingunge na kuongeza:

“Wanaacha kuzungumzia mambo ya msingi kama ufugaji na kuangalia masuala ya ufugaji jinsi ya kuwasaidia wasihamehame na kuwajengea mazingira mazuri ya kuendeshea ufugaji.” 

Hata hivyo, Kingunge aliwabeza watu wanaodai wananchi wa Mtwara ni wabinafsi, kwani wanaosema hivyo hawajui kama wakati wa mapigano ya uhuru walivyofanya kazi kubwa.

“Siwaungi mkono watu wanaosema  watu wa Mtwara ni wabinafsi, hao hawajui kama wakati wa vita watu wa Mtwara ndiyo waliofanya kazi kubwa kupigania uhuru,” alisema.

Naye Mwenyekiti wa Viongozi Wanawake Mtwara Vijijini, Maimuna Lipungu, alisema lengo la semina hiyo ni kutoa mawazo yao ya mwanzo kwa nafasi zao, angalau wapate elimu ili wananchi wajue mradi huo utakavyowanufaisha. MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top