Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Usichokijua kuhusu Askofu Moses Kulola

Askofu Kulola alizaliwa Juni 2, 1928 katika Kijiji cha Nyahonge wilayani Kwimba mkoani Mwanza. Ameacha mjane, watoto 10, wajukuu 44 na vitukuu 16. Alifungua makanisa zaidi ya 4,600 ya EAGT ndani na nje ya  Tanzania, ikiwemo Zambia, Malawi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo (DRC). Lakini ana nyumba moja tu aliyojengewa na waumini. 
*********
Ni vigumu kuzungumzia historia ya vuguvugu la uanzishaji makanisa nchini, pasipo kumtaja Askofu Moses Kulola.
Askofu Kulola anajulikana na wengi kama mtu aliye na nia ya dhati kutangaza neno la Mungu, kutokana na kile kinachoonekana wazi kwamba hakujilimbikizia mali kama ambavyo tunaona baadhi ya watumishi wa Mungu siku hizi wanavyomiliki majumba, benki na hata magari ya milioni ya shilingi.
Hali halisi
Kwa namna inavyoonekana nchini, ni kama kuna kundi kubwa la watumishi wanaohubiri kwa lengo la kushibisha matumbo yao zaidi; Hawana mpango thabiti wa kusaidia yatima wala maskini, badala yake waumini ndio wanaonyonywa kwa kutoa zaka na sadaka ambazo baadhi yake hata matumizi yake yamekuwa yakizua maswali.

Utumishi wa Mungu na mali
“Hakuna shaka kwamba kama kila nyumba ya ibada Tanzania ingekuwa na mpango thabiti wa kusaidia watu maskini, yatima na watu wengine wenye hali ngumu, hali ya maisha ingekuwa nzuri zaidi kwa wengi. Lakini wapi, baadhi ya watumishi wako ‘bize’ kujaza matumbo, wanaendesha magari ya kifahari yenye thamani ya mamilioni ya shilingi badala ya kutumia fedha hizo kutangaza neno la Mungu au kusaidia wasiojiweza,” anasema Charles Mtanga, mkazi wa Mbezi, Dar es Salaam.
Mtanga anawashauri viongozi wa nyumba za ibada kuwa na mkakati wa kusaidia yatima na watu wengine wasio na uwezo, huku wakiendelea kutangaza neno la Mungu, ili wote waweze kuufurahia ulimwengu.
Utanuzi wa huduma
Kwa  mujibu  wa  Askofu wa EAGT Sengerema, Joshua Wawa, Askofu Kulola alizaliwa Juni 2, 1928 katika Kijiji cha Nyahonge wilayani Kwimba mkoani Mwanza. Ameacha mjane, watoto 10, wajukuu 44 na vitukuu 16.
Katika uhai wake, Askofu Kulola alifungua makanisa 4,600 ya EAGT ndani na nje ya  Tanzania, ikiwemo Zambia, Malawi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo (DRC) na ameacha wosia kwamba makanisa yafunguliwe kadiri inavyowezekana.
Hata hivyo, licha ya kuwa na wingi wote huo wa makanisa, Askofu Kulola anamiliki nyumba moja iliyoko mkoani Mwanza aliyojengewa na waumini. MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top